Serikali isikie kiliochetu Walemavu;

Katibu wa chama cha walemavu Bw: Robart Masunga ameiomba Serikali kutoa kipaumbele kwa watuwanaoishi na ulemvu ili kuweza kuijikomboa kiuchumi, kisiasa na kitamaduni kwani wamesaurika .
Katibu huyo ametoa kauli hiyo jana kipindi akiongea na gazeti hili kuhusu mpango ambao anategemea kuanzisha kwa lengo la kufikisha ujumbe kwa jamii ili walemavu hao waweze kusaidiwa
Alisema kuwa wanampango wa kuzunguka katika kata saba huku wakifanya midaharo mbalimbali na kuelimisha walemavu kuhusu haki zao kwa lengo la kuwafumbua macho.
“Nia yetu kubwa ni kuzungunguka Maeneo ya vijijini kwani takwimu kubwa ya walemavu hawajapata Elimu kuhusu haki zao za msingi na Serikali imetusahau japo Mashirika mbalimbali ndo yanazidi kutupa vipaumbele” alisema Katibu huyo.
Aidha Bw: Robert alisema kuwa wanafunzi kutoka katika vyuo mbalimbli hapa nchini wamekuwa wakiwasilisha matatizo yao ili waweze kusaidiwa kupitia chama hicho lakini wanakwama kwa sababu mfuko wao hauna pesa za kiutosha.
“Tuna mpango wa kuomba msaada kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Venance Mwamengo pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Athuman Akalama na Mbunge wa Jimboletu waweze kutusaidia ii kutunisha mfuko wetu na kufanikisha lengo letu la ziara ya mafunzo kwa walemavu ususani maeneo ya vijijini” alisema.
Hata hivyo Katibu huyo aliongeza kuwa baada ya Halmasgauri kuwa mbili kuna haja ya kusajiri chama cha walemavu kupitia Halmashauri ya Mji wa Tarime baada ya kuzaliwa kutoka Halmashauri yaWilaya ya Tarime ili kiweze kupewa kipaummbele katika kupata Misaada kama vyama vingine hapa nchini.
Mwisho amezidi kutoa kili hata kwa mashirika mbalimbali yenye kutetea haki za walemavu kuzidi kupaza sauti ili serikali kusikia kilio chao ususani kwa sasa katikamchakato wa kutafta katiba Mpya.
“Nasisi tuna haki ya kutoa maoni yetu kama watu wengine ukizingatia vijjini hizi fursa zikija zinaishia maeneo ya Mjini na webngine je na wakati kura nyingi zinatoka vijijini” alisema
Powered by Blogger.