Madiwani wachachamaa kudai waraka ili kupata viko vitatu
Madiwani
wachachamaa kudai waraka ili kupata viko
vitatu
MKURUGENZI wa halmashauri ya Mji wa Tarime
Venance Mwamengo hivi karibuni amekwepa rungu la Madiwa wa halmashauri hiyo
kumtaka kufanya vikao 3 vya Baraza badala ya vikao 2 kwa sasa swali ambalo
liliibuliwa na Diwani kata ya Sabasaba Chirstoph Chomete.
Aidha Mkurugenzi huyo alidai mbele
ya baraza la madiwani kilicho fanyikia uwanja wa halmashauri Agost,01,2014 na
kusema kuwa hajapokea Waraka wowote kutoka Serikalini ambao unamruhusu kufanya
vikao vya Baraza 3 badala ya 2 kwa sasa na kuwa kufanya hivyo atakuwa amegeuka
maadili ya kazi.
''Hapa kwetu tunafanya
kikao cha Chama na kikao cha Baraza la madiwani lakini kikao cha Madiwani
kuwasilisha hali ya maendeleo ya kata yake hatufanyi kwa sababu hatuja pokea
Waraka wowote amabo unaniruhusu na nikipata waraka hiyo haina shida''alisema
Mwamengo.
Majibu hayo yalizua
mtafaruku katika kikao hicho ambapo madiwani walitaka kujua sababu ya kushindwa
kufuatilia waraka hata katika halmashauri zingine kama vile halmashauri ya
Tarime iliyo karibu na kuendana na wakati.
Akifafanua Chomete
alisema kuwa kuna haja halimashauri yake kuiga kutoka halmashauri zingi ambazo
zinaendesha vikao 3 badala ya 2 kama waraka unavyosema na kuongeza kuwa
Mkurugenzi asiendelee kung'ang'ania mfumo wa zamani ambao umepitwa na wakati
badala yake atafute waraka kutoka halimashauri zingine ambazo tayari zimekwisha
upata.
Chomete alitaja
Halmashauri amabazo tarari zimeingia katika mfumo wa kufanya kikao 3 badala ya
2 kama ilivyo kuwa hapo nyuma kuwa ni pamoja na halmashauri ya
Tarime,halmashauri ya Serengeti na hata halmashauri ya Musoma na kuwa
Mkurugenzi atafute waraka huo katika halmashauri hizo.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Daudi Wangwe aliwatuliza madiwani na kudai kuwa
atahakikisha analivalia njuga swala hilo na kuwa wanapata waraka ambao
utawaruhusu kuendelea kufanya vikao 3 kama halmashauri zingine.
''Hata mimi nina haja ya
kuwasilisha hali ya maendeleo ya kata yangu katika baraza hili lakini kutokana
na kuwa hatuja pokea Waraka wowote ambao Unaturuhusu kufanya vikao 3
hatutalazimisha kufanya bila kuwa waraka kwa hali hiyo tuendelee kuwa watulivu
wakati hatua zingine zinaendelea kufanyika na kuhakikisha kuwa tunaingia mfumo
mpya wa vikao''alisema Wangwe.
........................................................mwisho.....
........................................................mwisho.....