Wananchi waunganisha nguvu kudai fidia Maeneo yaliyofanyiwa Uthamini na Serikali:



Wananchi waunganisha nguvu kudai fidia Maeneo yaliyofanyiwa Uthamini na Serikali:

 Tarime:

WANANCHI wavijiji saba vinavyozunguka Mgodi wa Afrika Barrick Gold Mine wameungana pamoja katika swala zima la kudai fidia maeneo yote ambayo yamefanyiwa uthamini na Serikali.

Aidha Wananchi hao wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Tarime Nyambari Chcha Mariba Nyangwene walisema hayo    jana kwenye kikao chapamoja ambacho kiliwajumuisha viongozi wa vijiji hivyo kuwa wameondoa tofauti zao katika kudai swala zima la Fidia ya maeneo yao ambayo yamefanyiwa tathimini na serikali.

Akiongea Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mkoa Mara Nansy Msafiri katika kikao hicho ambacho kilikalia katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya Tarime,julai,30, 2014 alisema kuwa kunahaja Wananchi kuunganisha  nguvu ya pamoja katika swalazima la kudai haki ya fidia katika maeneo ambayo yamefanyiwa Uthamini na Serikali tayari kwa shuguli za Mgodi.

Aidha Msafiri aliongezaa kuwa kuna haja Mgodi kilipan fidia watu ambao wanaishi karibi na maenewo ya machimbo ambao wamo ndani ya umbali wa mita 200 na kuwa watu hao wanaadhirika na vumbi ikiwemo na matetemeko ya Baruti.

Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya Tarime Amosi Sagara alisema kupitia kamati ya kikosi kazi kilichoundwa na Wizara ya Ardhi halmashauri ilishinikiza Mgodi kilipa Fidia Wananchi.

‘’lmashauri ilishinikiza Mgodi kulipa fidia wananchi maeneo ambayo yamefanyiwa tadhimini na kikosi kazi ambapo Mgodi umelipa fidia Wananchi katika maeneo ya Nyakunguru,Kewanja,Nyangoto kwa awamu sita’’alisema Sagara.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya alisema kuwa Mgodi unatakiwa kulipa fidia wananchi ambao tayari wamefanyiwa Uthamini na wale ambao wako jirani na maeneo ya mcchimbo mita 200 ambapo hayo yapo kisheria.

‘’Wananchi tunahitaji kudai fidia kisheria na bila kushikana miguu na tuunganishe nguvu pamoja katika swala zima la kudai haki ya fidia maeneo ambayo yamefanyiwa uthamini sanjari na wale ambao wanaishi ndani ya mita 200 aidha kuna baadhi ya viongozi wachache ambao wanadai wananchi kitu kidogo endapo watakuwa  jambo  linapaswa kukemewa’’alisema Henjewele. 

Kwa Upande wake Diwani viti  maalumu katika kata ya Matongo Tarafa Ingwe Bi: Philomena Tontora alisema kuwaTangu mwaka 1982 wataalamu walifanya utafiti na kugundua kuwaeneo la nyamongo kuna pango refu linaloelekea Misiri pamoja na Mto unaoelekea Mto Tanganyika ndapo
Mgodi ukianzakuchimba kupita chini ya Ardhi maisha ya  Wananchi yatakuwa salama hivyo serikali iliangalie hilo mara moja ili kunusuru wananchi hao.

Naye Mbunge wajimbo la Tarime Nyambari Nyangwine katika  kikao hicho ambacha alikuwa Mwenyekiti alisema kuwa wananchi washirikiane na kuungana kwa pamoja kwa lengo la kupata haki zao.

“Tutaandamana kisheria ili kuweza kupata haki zetu sisi wana pia natoa agizo kwa Watendaji wa Vijiji,na Kata kuandaa kikao ili kuleta maoni ya wananchi kwa lengo la kuyawasilisha serikalini”alisema Nyambari.
                                              …..Mwisho…

Powered by Blogger.