Polisi fc walazwa kwa kichapo cha bao 2-1 didi ya Mafundi fc:



  Picha ya aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Tarime rorya SACP Justus kamugisha kulia akikabidhi kaputeni wa timu ya mafundi Fc Babu Matacha ngao ya ushindi baada ya kukabidhiwa zawadi ya shilingi laki moja baada ya kuilaza polisi fc Tarime kichapo cha bao 2-1 katika uwanja wa serengeti Mjini Tarime

 Timu ya polisi Fc Tarime imelazwa kichapo cha bao 2-1 dhiodi ya Mafundi Fc Tarime katika michuano ya kumwaga aliekuwa kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa kipolisi Tarime Rora SACP Justus Kamugisha katika viwanja va Serengeti Mjin Tarime.

Katika mashindano hayo ambayo yamewakutanisha watani wa jadi hao wawili kipindi cha  kwanza mchezo huo waliweza kutoana jasho mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika walitoka bila ya kufungana na ndipo kipindi cha pili dk ya nne Mfundi fc walichungulia nyavu za polisi fc kupitia kwa Barnabas Wilibard na kudumu mpa dakika ya  72 ndipo polisi fc kupitia kwa  Godfrey Francis alisawazisha.

Mtanange huo ulizidi kutoana jasho ndipo kipindi cha dk 76  Thomas Marwa alipachika bao na kusababishia mafundi kujinyakulia ushindi huo.

Katika Mashindano hayo mshindi wa kwanza ambaye ni Mafundi Fc walipewa zawdi ya shilingi, 100,000 na Ngao ya Ushidi na mshibdi wa pili Shilingi 50,000.

Kwa upande wake kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa kipolisi ambaye kwa sasa amehamishiwa mkoani shinyanga aliwataka wanamichezo hao pamoja na wadau wa michezo kuzidi kudumisha michezo wilayani Tarime pamoja nakutoa Ushirikiano wa kutosha kwa kamanda mpya ili kuboresha soka wilayani Tarime.

“Nitaendelea kuwasaidia katika michezo lakini  kuweni na Ushirikiano wa kutosha” alisema kamanda.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mpira willaya TAFA John Rutente aliwaimiza wachezaji hao kuendeleza soka ili kuweza kuibua vipaji vya kutosha ndini ya wilaya.
“Vipaji tunavyo vya kutosha kikubwa ni kuzidi kuwekeza katika suala zima la soka wilayani hapa” alisema Mwenyekiti Tafa.
               …….MWISHO….

Powered by Blogger.