Nyabigena yanufaisha vijana.




Nyabigena ni Ushirika uanaounganisha vijana kutoka katika vijiji saba vinavyozunguka mgodi wa dhahabu wa Nyamongo African Barrick Gold Mine (ABG).

Ushirika huo umeweza kupata tenda mbalimbali katika mgodi wa dhahabu wa Nyamongo kama vile kufagia ndani ya mgodi, kukusanya vyuma chakavu, na kupulizia dawa ya ukoko kwa ajili ya kuua mazalia ya ili kutokomeza maralia.

Kupitia kazi hizo vijana mbalimbali kutoka katika vijiji saba vinavyozunguka mgodi huo wameweza kupata ajila za moja kwa moja kupitia ushirika huo wa Nyabigena.

Kirigiti Sasi ni katibu wa ushirika huo alisema kuwa ushirika huo una jumla ya wafanyakazi  917 ambao wameweza kupata ajila kupitia Miradi mbalimbali inaoendeshwa na Ushirika huo wa Nyabigena  huku Ushirika wa Saccos ukiwa na Wafanyakazi, 122, 300   walinzi na140 wakifanya   kazi mbalimbali kupitia uhirika huo na 80 ni wafanyakazi wa viwanda vidogo vidogo Sido.

“Kupitia Barrick ushirika wetu umeweza kuanzisha miradi mbalimbali na kuajili kila rika na vija tumeweza kuwapa kipaumbele” alisema Kiriiti.

Hata hivyo katibu wa ushirika huo aliongeza kuwa Licha ya  kuwa na ushirika huo kuwapa vijana vipaumbele katika ajila wameweza kuunda pia ushirika wa kuweka na kukopa ili kuweza kuwakopesha wanachama wake huku wakisaidia watoto wanaoishi katika mazinigira hatarishi na Walemavu.

“Watoto wasiojiweza tunawasaidia kuwalipia karo ili kudumisha mhusiano yetu na wananchi kutoka katika vijiji saba vinavyozunuka modi wetu” alisema katibu.
                                                 …..Mwisho….


Powered by Blogger.