Mchungaji azidi kukemea vitendo vya ukatili

Mchungaji azidi kukemea vitendo vya ukatili
 

 
Mchungaji wa kanisa la Evanjeristi Assembly of god Thomas Rioba amezidi kukemea vitendo vya ukatili wa kijnsia dhidi ya mama na mtoto ambavyo vimekuwa tishio kubwa vinavyozidi kutendeka katika jamii wilayani hapa vikiwemo vya kuchomwa kwa moto, kuawa na kutolewa kwa baadhi ya viungo vya binadamu pamoja na kujeruhi kwa mapanga  waweze kubadilika ikiwa ni pamoja na kuondokana na mitazamo hasi ili kuweza kumrudia mwenyezi mungu.
 
Mchungaji huyo alizidi kuitaka jamii ya kikurya kuondokana na mila potofu ambazo  zinazidi kukandamiza mtoto wa  kike na kumukosesha haki zake za msingi kama vile Elimu.
 
“Tumekuwa tukishudia matukio mbalimbali wanayotendewa ndugu zetu hivyo tufikie hatua na kumwogopa mwenyezi mungu ili kutangaza wilaya yetu kwa mazuri” alisema mchungaji huyo.
 
Naye  mkurugenzi mtendaji wa haki za binadamu wilayaniTarime Mkoani Mara (SHEHABITA) Bonny Matto ameitaka jamii  kuondokana na suala zima la kujichukulia sheria mkononi ikiwa ni pamoja na kufuata sheria zilizopo ili kuishi kwa amani.
 
Aliongeza kuwa suala la kukiuka sheria ndo chanzo kikubwa na kisababishi cha uvunjifu wa amani ambao unasababisha vitendo vya ukatili wilayani hapa.
 
“Jamii kwanza ibadilike ili tuweze kutokomeza vitendo vya ukatili iliwa ni opamoja na wazazina walezi kukubali  mabadiliko kwa sasa tumezanzisha mafunzo juu ya athali za ukatili katika wilaya ya Tarime na Rorya ili kutokomeza vitendo hivi” alisema Mkurugenzi.
Kwa upoande wake mratibu wa shirika la jukwaa la Mtoto (CDF) Restuta mpate aliwaomba wazee wa kimira pamoja na viongozi wa serikali za vijiji  kuungana pamoja ili kutokomeza vitendo hivyo.
 
Ameongeza kuwa endapoa jamii ya vijiji ikiondokana na ukimya itasaidia kupunguza vitendo hivyo vya ukatili na kuweza kubaini watuhumiwa wa vitendo hivyo ili kuchukuliwa hatua za kisheria.
 
Kwa upande wake mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake (Tamwa) Valerie Msoka amezidi kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyozidi kutokea wilayani humo.
 
“Jamii iondokane na mambo ya kumnyanyasa  mtoto wa kike pamoja na udhalilishaji ili mwanamke hawreze kuijikomboa tunaendelea kutoa elimu kwa vyombo vya habari ili vizidi kupaza sauti kwa lengo la kukomboa mwanamke” alisema.
 
Sanjari na hayo serikali kupitia halmashauri za Wilaya ya Tarime na Mji wa Tarime hawana budi kuhunda mbinu mbadala ili kukomesha vitendo vya ukatili wilayani humo.
 
                                      …..Mwisho…
Powered by Blogger.