WAWILI WAJERUHIWA MAPANGA.
WAWILI WAJERUHIWA MAPANGA.
BARIADI
Watu
wawili wamevamiwa na kujeruhiwa kwa mapanga na watu wasiofahamika katika
kijiji cha Ditima kata ya Guduwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu na
kukatwakatwa mapanga kisha watu hao kutokomea kusikojulikana.
Akiongelea
tukio hilo ,esther jali ambaye ni mmoja wa majeruhi
alisema majira ya saa moja usiku wa kijiandaa kula chakula na
mama yake , ghafla walivamiwa na watu wasiofahamika na kuanza kushambuliwa.
Walianza
kumkata mama kikongwe mwenye umri wa miaka 80 kichwani na shingoni ,kisha
kumkata panga binti yake mkono wa kulia, wakati akijaribu kumsaidia mama
yake kwa kelele za kuomba msaada watu hao walitoweka eneo hilo.
Naye
kijana wa mama huyo Daudi Kabale alisema alisikitishwa sana
na kitendo hicho cha kikatili ambacho kinawaweka wakinamama katika hali
ya wasiwasi na kuiomba serikali kuingilia kati suala hilo.
Kwa
upande wake mganga wa zamu ktk hospitali ya wilaya ya bariadi Revocatus Nkumbi
alikiri kupokea majeruhi hao , wakati mmojawapo akiwa ameishiwa damu kutokana
na kuvuja damu nyingi ,hivyo juhudi za kuyaokoa maisha yake zimefanikiwa.
“Tulipokea
majeruhi hao wawili hospitalini hapa na harakati za kuokoa maisha yao
zinaendelea kufanyika ili kuyanusuru maisha yao”, alifafanu mganga Nkumbi.
Kaimu
kamanda wa polisi wa mkoa wa simiyu Venance Kimario alithibitisha kutokea
kwa tukio lilo na kwamba uchunguzi wa kuwasaka watu hao unaendelea ili
kuwafikisha mahakamani juu ya tukio hilo.