Tarime watakiwa kufichua vitendo vya ukatili wa kijinsia:

Vijana wakitoa Maigizo yenye ujumbe kuhusu madhara yatokanayo na hathari za ukeketaji, Ndoa za utotoni, pamoja naMimba za utotoni katika tamasha la kupinga ukatili wa kijinsia lililoandaliwa na TGNP mtandao hivi karibuni na kufanyika katika shule ya msingi Ng'ereng'ere kata Nyamaraga wilayani Tarime Mkoani Mara takribani siku tatu huku zikijadiliwa mada mbalimbali kwa lengo la kubadilisha jamii.



Tarime watakiwa kufichua vitendo vya ukatili wa kijinsia:

Jamii imetakiwa kufichua vitendo vya ukatili vinavyozidi kutendeka maeneo mbalimblai wilayani humo kwa serikali, Taasisi za watu binafsi,mashirika kwa lengo la kutokomeza vitendo  hivyo.

Kauli hiyo imetolewa na Ofisa tawala Bw: Baraka Nyamsenda kwa niaba ya mkuu wa wilya ya Tarime John Henjewele katika ufunguzi watamasha la kupinga ukatili wa kijinsia, Ukeketaji, Ndoa za utotoni  lililofanyika katika shule ya msingi ng’ereng’ere  kata Nyamaraga wilayani Tarime Mkoani Mara.

Mgeni rasmi alisema kuwa jamii kwa ujumla iondokanae nasuala la kuwaficha wale wanausika katika kutenda unyama kwa wakina mama, watoto wa kike kwa kushirikiana na serikali  ili kuweza kuwachukulia hatua mara moja na kutokomeza vitendo vya kikatilia wilayani Tarime.

“Siri mlizonazo ndo zinazidi kutupa changamoto kwa mashirika Halmashauri kwakushirikiana na mkuu wa wilaya tupo bega kwa bega kupinga vitendo hivyo” alisema mgeni rasmi.

Merry msemwa ni meneja wa  programu  katika uanarakati, Utafiti na Ushawishi pamoja na Utetezi katika TGNP Mtandao katika tamasha hilo alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa tamasha hilo ambalo litachukua takiribani siku tatu nikuweka mikakati mahususi ili kila mtu kuweza kupata fursa ya kushiriki tamasha hilo na kutoa mawazo yake.

“Matamasha haya tumekuwa tukiyafanyia Dar –es salaam lakini mwaka huu tumeamua kufika kwa walengwawenyewe wanaokumbwa na masula ya ukatili wa kijinsia” alisema Mery.

Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za wanawake  la kivulinilililo po jijini mwanzaBi: Maim una Kanyamala  katika kutoa mada halisi juu yua ukeketaji na ndoa za utotoni  mbele ya mgeni rasmi alisema kuwa wameamua kuongelea mada hiyo kwa sababu wanajali utu wa jamii nzima bila kujali  umri, elimu,dini,na itikadi ya vyama.

Aliongeza kuwaMkoa wa mara ni  kati ya mikoa mitatu nchini inayoongoza kwa  kiwango kikubwa sana katika ndoa za utotoni, nakusema kuwa takwimu za kitaifa zinaonesha zaidi ya nusu ya wasichana wadogo wanaozwa. Mikoa mongine ni Shinyanga asilimia59% Taboraasilimia58% ikifuatiwa Mara55%.

Aidha ameongeza Takwimu za Mwaka 2010 za DHS  zinaonesha katika kanda ya ziwa Mara iko chini  sana kwa matumizi ya uzazi wa mpango kwani asilimia9.8 tu wanawakeutumia uzazi huo wa mpango.

Hata hivyo mkoa wa mara kwa takwimu za mwaka 2010 asilimia 72% inaongoza katika vitendo vya ukatili wa kimwili na kijinsia ikifuatwa Dodomaasilimia 71, na ya tatu pemba asilimia 05,

Sanjari na hayo imeonekana kuwa sheria ya ndoa  ya mwaka 1971 haiwalindi watoto watoto wa kike wenye umri chini ya miaka18dhidi ya kuolewa bali sheria hiyoinaruhusu wasichana wenye umri wa miaka 14 kuolewa kwa ridhaa maalum na mara nyingi uruhusu wasichana wa miaka 15 kuolew kwa ridhaa ya wazazi wao hali ambayo inazidi kuathili maendeleo ya motto wa kike.

Hivyo mkurugenzi huyo alisema kuwa serikali haina budi kurekebisha sheria hiyo ili kuwalinda watoto wa kike.




Powered by Blogger.