Waandishi wa habari watakiwa kuandika habari zenye ukweli

Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA Bi: Valeria Msoka akiongea na waandishi wa habari katika semina inayoendelea jijini Mwanza kwenye ukumbi wa Midlkand Hotel kwa lengo la kuzungumzia vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya mama na mtoto kulia kwake ni mkurugenzi wa UTPC Bw:Abubakar Karsan

                                                                 Mwanza

Waandishi wa habari wametakiwa kuandika habari za kweli na si kuandika habari zenye uchochezi ambao unaweza kuvuruga amani ya Tanzania

Kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi mtendaji wa UTPC Bw:Abubakar Karsan katika ufunguzi wa mafunzo ya waandishi wa habari kutoka  katika mikoa mitano ya kanda ya ziwa yaliyoandaliwa na chama cha  waandiishi wa habari wanawake Tamwa na kufadhiliwa na (UNFPA) yanayo fanyika katika ukumbi wa Midland hoteli jijini Mwanza kwa takribai siku tatu.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa waandishi wa habari  wasimamie ukweli kwa lengo la kubadilisha jamii na si kukalia kuandika habari za kiuchochezi zenye maslahi ya watu binafsi.

“Tumieni vizuri fursa mnazozipata kwa lengo la kubadili jamii inayowazunguka pia waandishi ondokana na suala la kulazimisha posho” alisema Mkurugenzi.

Kwa upande wake mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari Varelia Msoka alisema kuwa waandishi wa habari waendelee kuibua mambo ambao yamejificha  lengo la kuleta mabadiliko.

“Kupitia TAMWA tunazidi kupambana kwa kushirikiana na  Mashirika mengine lakini bila nguvu ya  waandishi wa habari ujumbe tuliokusudia hautafika maeneo huska” alisema Msoka.

Hata hivyo mkurugenzi huyo aliongeza kuwa Mafunzo hayo ambayo yatakuwa takribani siku tatu kwa waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Kagera,Mara na Simiyu kwa lengo la kupata mafunzo juu ya kuandika habari za  ukatili wa kijinsia dhidi ya mama na  mtoto.


Aidha mkurugenzi huyo alisema kuwa waandishi hao wasimamamie ukweli na kuibua vitendo vya ukatili ambavyo vimeshamiri ususani mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara ili kuweza kuleta mabadiliko.

Washiriki wa mafunzo hayo walisema kuwa watakuwa mstali wa mbele kwa lengo la kuzidi kuibua changamoto zilizopo vijijini ili kuleta mabadiliko.

Powered by Blogger.