Nyambari akemea siasa Mashuleni:

Nyambari akemea siasa Mashuleni:
 

Mbunge wa jimbo la Tarime Nyambari Nyangwine amekemea sula la siasa mashuleni kwa lengo la kunusuru wanafunzi ili kuongeza ufahuru  wao.
 
Kauli hiyo ilitolewa jana kipindi akiongea na vyombo vya habari kuwa baadhi ya walimu   na wanafunzi wamekuwa wakiendesha suala zima la siasa  shuleni .
 
Nyambari alisema kuwa baadhi ya walimu wamekuwa kichocheo kikubwa cha kuanzisha suala zima la siasa mashuleni na kupelekea wanafunzi  kufeli masomo kwani walimu  hao utumia muda mwingi kujadili mambo ya siasa na kupoteza muda wa kufundisha masomo yao.
 
Natoa mwito kwa walimu wote kuondokana mara ,moja na  mambo ya kisiasa mashuleni pia walimu wawe wakali kwa ajili ya kuwakanya wanafunzi ambao wanajiingiza katika masuala ya kisiasa na  mwisho wake kufeli masomo alisema Nyambari.
 
Aidha mbunge huyo aliongelea suala zima la njaa ambalo limekumba baadhi ya kata na kusema kuwa watendaji wa vijiji wawe wazi katika kutoa taarifa sahii ili kuwa na takwimu nzuri za kubaini familia zilizokumbwa na njaa ili ziwezekupata msaada wa chakula mara moja.
 
“Watendaji hawatoi takwimu sahii ili tipate familia sahii zenye mahitaji suala ambalo ni changamoto kwetu”alisema mbunge.
 
Hata hivyo mbunge huyo wa jimbo la Tarime amekemea vitendo vya jeshi la polisi amabavyo vinatendeka ususani kunyanyasa raia, kubandikia kesi waondokane navya mara moja.
 
“Mtu  yeyote anayenyanyasa masikini lazima nipambane naye kila raia anahaki ya kupata huduma nzuri na si kunyanyaswa tunataka Tarime byenye Amani, Upendo. Ushirikiano pamoja na Mshikamano” alisema Nyambari.
 
Mwisho mbunge amekemea baadhi ya watu ambao wameanza kampeni zao mapema wasije wakasababisha uvunjifu wa amani pia waondokane na kutumia vibaya vijana kwa ajili ya uchochezi wa vujo.
Powered by Blogger.