Diwani wa kata ya Ikoma ahamasisha michezo

Diwaini wa kata ya ikoma wilayani Rorya mkoani Mara Laurent Adriano akiongea na wananchi wake kuhusiana na michezo





Diwani wa kata ya Ikoma wilayani  Rorya mkoani Mara Laurent Adriano amehamasisha suala la michezo wilayani humo kwa lengo la kuwabadilisha mitazamo hasi vijana waliyonayo.

Diwani huyo alisema kuwa suala la michezo ni ajira hivyo vijana hao hawanabudi kulitililia mkazo kwa lengo la kujiaji;li wenyewe na si kusubili kaujiliwa na serikali ikiwa ni pamoja na kudumisha Upendo, Amani pamoja na ujirani mwema baina ya kata jirani kupitia michezo hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na diwani hiyo katika kukabidhi zawadi za kombe la Adrian Cup 2014-2015 lililokuwalikishindaniwa   katika uwanja wa kogaja  huku  timu kumi na moja kutoka katika vijiji vitatu vilivyomo ndani ya kata ya ikoma wilayani Rorya zikishiriki mashindano hayo,

“Lengo langu la kuanzisha mashindano haya ni kuhamasisha vijana kupenda michezo hivyo naomba mudumishe michezo na tusiishie hapa tuweza kupata timu mbili na kushiriki ngazi ya mkoa hadi Taifa” alisema Diwani.

Katika michuano hiyo Timu ya Young Stars iliibuka kidedea baada ya kuichapa timu ya Lwanda fc kibao cha 1-0 ambapo bao lilifungwa na George Bededict dakika ya 15 kipindi cha kwanza ambapo iliweza kudumu mpaka dakika za mwisho.

Mshindi wa kwanza mpaka wa tano waliweza kupata zawadi mbalimbali amabapo mshindi wa kwanza alipewa shilingi laki nne na elfu themanini na seti moja ya jenzi, mshindi wa pili laki tatu na elfu themanini, mshindi wa tatu  laki mbili na elfu themanini, mshindi wa nne laki moja na elfu themanini na mshindi wa tano alipwewa shilingi laki mija na elfu thelathini huku kuanzia mshindi wa sita mpaka timu ya kumi na moja ikipewa zawadi ya shilingi elfu themanini kwa kila timu.

Katika fainali hiyo mgeni rasmi alikuwa mkuu wa chuo cha uhasibu kilichopo Arusha Prof Johannes Monyo ambapo alihaidi kwa kila timu kutoa seti ya jenzi ili kuweza kudumisha michezo wilayani humo.

“Nimetoka mbali kuja kushudia michuano ya Adrian Cup 2014-2015 kwa lengo la kuwapa vijana moyo ili wapende mochezo kwani michezo ni ajira tumieni fursa hizo za michezo vizuri na msibadilishwe na wachache wenye nia yao binafsi” alisema Profesa Monyo.

Hata hivyo mgeni rasmi huyo alimwomba diwani huyo kutoishia hapo bali vijana waendelezwe katika suala zima la michezo huku wakitafutiwa wafadhili
                      …….Mwisho….
Powered by Blogger.