Vijana wanaozunguka mgodi wa Barrick wapewa mafunzo ya ujasiliamali:

Nick wa pili akitoa mada kwa vijana kutoka vijiji saba vinavyozunguka mgodi wa dhahabu wa Nyamongo wilayani Tarime Mkoani Mara katika semina ya mafunzo ya ujasiliamali na kujua utumiaji wa fursa walizonazo

 
 
Vijana zaidi ya miambili kutoka katika vijiji saba  vinavyozunguka mgodi wa dhahabu wa Norht Mara  wa African Barrick Gold Mine (ABG) uliopo Nyamongo wilayani Tarime Mkoani Mara wamepata mafunzo ya  utumiaji wa fursa zilizopo kwa lengo la kujikomboa kiuchumi.
 
Mafunzo hayo yameanza Julai 4 na kuitimishwa Julai 5 Mwaka huu  katika shule ya sekondari Ingwe huku yakidhaminiwa na   Mgodi wa North Mara pamoja na Clouds Media Group ili vijana waweze kutambua umuhimu wa fursa zilizopo kwa lengo la kuwanufaisha kimaisha.
 
Katika mafunzo hayo zimekuwa zimejadiliwa mada kama vile jinsi ya kufanya ujasiliamali wenye tija, Elimu juu ya matumizi ya fedha,Elimu ya Afya,Nidhamu ya Mafanikio uwapo kazini, Namna ya  kubuni na kuzitambua kwa manufaa ya kuzitumia katika kuboresha maisha , Na jinsi ya kupata masoko na kuyatumia.
 
Aidha vijana hao katika kuwasilisha mada wameuomba mgodi huo kuwapa maeneo ya uchimbaji mdogo kwa lengo la kujipatia kipato na kusema kuwa mafunzo hayo yamewafumbua macho  kwa sasa.
 
“Tumekuwa tukishindwaz kutumia vizuri fursa zetu na rasilimali tulizonazo kwa kukosa elimu tuliyoipata nadhani tutafanya mapinduzi” walisema washiriki hao.
 
Katika kutoa mafunzo hayo Msanii maarufu wa mziki wa hip hop  Nick wapili amewataka vijana hao kulipa kipaumbele suala la Elimu ili waweze kuijikomboa wao na kuwataka vijana hao kutumia vizuri mitandao ya kijamii kwa lengo la kunufaika
 
“Mitandao ya kijamii ukiitumia vizuri nfano katika kusoma unaweza kunufaika lakini vijana waliowengi mnatumia  mitandao hiyo tofauti suala ambalo limewakumba vijana wengi na kupoteza mwerekeo wa maisha” alisema Nick wa pili.
 
Budeki John kutoka katika kijiji cha Nyangoto alisema kuwa fursa hiyo ya kupata mafunzo hayo kwao imekuwa bahati kubwa hivyo amewataka vijana wenzake kutambua fursa hizo na kuzitumia vizuri  kwa lengo la kunufaika kimaisha na kubadili mitazamo waliyonayo ya kuvamia mgodi huo mara kwa mara ili kupata mawe ya dhahabu.
 
“Vijana tuvamia mgodi na kupata fedha nyingi lakini tunazitumia vibaya kupitia elimu tuliyoipata vijana watabadilika” alisema Budeki.
 
Nikodemus Keryaro ni ofisa ushirikishwaji alizitaja  changamoto zinazokumba jamii inayozunguka mgodi huo kuwa hawako tayari kutumia vizuri fursa hizo wanazozipata kwa lengo la kubadilika na kuongeza uchumi.
 
“Tulitegemea kupata vijana zaidi ya miasita kutoka vijiji saba vya mgodi lakini idadi iliyopo ni chache na wengine wapo darasani lakini hawazingatii masomo hayo na ni wachache watakao yafanyia kazi” alisema Nicodemus.
 
Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii kutoka African Barrick Gold Mine (ABG) North Mara BeatriceThobias aliitaka jamii kutumia ipasavyo fursa kama hizo kwani fursa hizo zimefika maeneo ya vijini na kuongeza kuwa fursa hizo zimeanza kufika maeneo ya vijijini hivyo jamii iondikane na dhana potofu ambayo imejijengea kwa lengo la kuleta mabadiliko.
 
“Fursa hizi zimekuwa zikitoka maeneo ya mjini na jamii inachangila lakini hapa jamii inapata  mafunzo bure kupitia Mgodi huu na Cluds Media Group bado mwitikio ni mdogo sana inabidi jamii kubadilika na kuchangamkia fursa hizi mara moja” alisema Beatrice.
Powered by Blogger.