Mashirika elekezeni nguvu kubwa vijijini:



Mashirika elekezeni nguvu kubwa vijijini:

MAKALA:
Mashirika mbalimbali yamekuwa mstari wa mbele kwa lengo la kutokomeza suala zima la ukatiki wa kijinsia ambao umekuwa tishio katika mikoa mbalimbali dhidi ya mama na motto.

Katika tamasha la kupinga  ukatili wa kijinsia dhidi ya akinamama na mtoto lililofanyika  hivi karibuni katika  shule ya msingi Ng’ereng’ere kata Nyamaraga Wilayani Tarime mkoani Mara  imebainika kuwa mkoa wa Mara unaongoza kwa ukatili wa kimwili dhidi ya mtoto wa kike kwa  asilimia72 ukifuatiwa na mkoa wa Dodoma wenye asilimia71 na mkoa wa Pemba wenye asilimia  05 huku mashirika yakizidi kupambana na suala hilo kwa lengo la kumkomboa mtoto wa kike.

TGNP Mtandao umeweza kubainisha takwimu hizo za mwaka 2010 katika tamasha  lililoandaliwa likichukuwa takribani siku tatu huku mada mbalimbali zikiongelewa kwa lengo la kufikisha ujumbe  katika jamii.

Kongamano,Mbalimbali za kupinga ukatili huo zimekuwa zikifanyika maeneo ya mjini na si vijijini wakati waanga wakubwa wako maeneo ya vijijini suala amabalo bado ni changamoto kwa mashirika hayo lakini kwa kutambua umuhimu wa mtoto wa kike mashirika hayo yameweza kuunganisha nguvu za pamoja na kufika maeneo ya vijijini  kwa lengo la klutoa semina na mafunzo mbalimnbali juu ya kupinga ukatili dhidi ya mamana mtoto, Ndoa za utotoni, ukeketaji pamoja na Mimba za utotoni.

Tumekuwa tukiona juhudi za chama cha waandishi wa habari wanawake (Tamwa) kupitia mkurugenzi wake Varelia Msoka wakiunganisha nguvu ya pamoja kwa lengo la kumlinda mtoto wa kike pale anaponyimwa haki yake, anaponyanyaswa aidha kingono, kiakili mashirika hayo uinesha juhudi za makusudi kwa lengo la kuleta mabadiliko katika sehemu  husika.

Hata hivyo chama cha waandishi wa habari  wanawake(TAMWA)kimekuwa pia na juhudi za kutoa mafunzo mbalimbali kwa waandishi wa  habari ili kuwajengea uwezo na uelewa pamoja na ujasili wa kuendelea kuandika vitendo vya ukatili ili jamii kuweza kubadili mienemndo na mitazamo waliojijengea.

Juhudi  hizo za mashirika mbalimbali, CBO,NGOS, CSO zimeweza kusaidia kupunguza vitendo hivi vya ukatili kwa kiasi fulani japo waanga wengine hawajafikiwa kulingana na mazingira waliyopo hivyo serikali kwa kuunganisha nguvu za pamoja hawana budi kufika maeneo ya vijijini ili kuokomesha vitendo hivyo vya kikatili.

Kwa upande mwaingine vitendo hivi nanaonekana kukua kwa kasi ni baada ya jamii kupata elimu za kutosha na kuanza kutoa taarifa kwa vyombo husika na kufanyiwa kazi kwani awali vitendo hivyo vilikuwa vikitendeka na jamii inakaa kimya.

Ndoa za utotoni,Mkoa wa Marani kati ya mikoa  mitatu nchini Tanzania ambayo inaongoza kwa kiwango kikubwa saa cha ndoa za utotoni takwimu za kitaifa zinaonesha zaidi ya nusu ya  wasichanae wadogo wanaozeshwa mikoa minginea ni pamoja na Shinyanga asilimia59% Tabora58% ikifuatiwa Mara asilimia55%  na uku utafiti ukionesha mkoa wenye asilimia ndogo katika suala zima la ndoa za utotoni Iringa 08%.


Merry msemwa ni meneja wa  programu  katika uanarakati, Utafiti na Ushawishi pamoja na Utetezi katika TGNP Mtandao katika tamasha hilo alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa tamasha hilo ambalo litachukua takiribani siku tatu nikuweka mikakati mahususi ili kila mtu kuweza kupata fursa ya kushiriki tamasha hilo na kutoa mawazo yake.

“Matamasha haya tumekuwa tukiyafanyia Dar –es salaam lakini mwaka huu tumeamua kufika kwa walengwawenyewe wanaokumbwa na masula ya ukatili wa kijinsia” alisema Mery.

Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za wanawake  la kivulinilililo po jijini mwanzaBi: Maimuna Kanyamala  katika kutoa mada halisi juu yua ukeketaji na ndoa za utotoni  mbele ya mgeni rasmi Ofisa Tawala wa wiliya Baraka Nyamsenda kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Tarime John Henjewele alisema kuwa wameamua kuongelea mada hiyo kwa sababu wanajali utu wa jamii nzima bila kujali  umri, elimu,dini,na itikadi ya vyama.

Mgeni rasmi huyo alitoa mwito ka jamii kuwa waweze kufichua jamii ambayo inazidi kukumbatia vitendo hivyo vya kinyama kwa lengo la  kupunguza ukatili huo ndani ya wilaya ya Tarime.

“Siri mnazotunza kwa  watu wanaotenda unyama huo ndo  changamoto kwa mashirika Halmashauri kwa kushirikiana na mkuu wa wilaya tupo bega kwa bega kupinga vitendo hivyo toeni taarifa vyombo vya sheria viko wazi” alisema mgeni rasmi.

  Hta hivyo Mkoa wa Mara kwa kanda ya ziwa takwimu za mwaka2010 za DHS zilionesha kuwa Mara iko chini sana  kwa matumizi ya uzazi wa mpango kwani ni asilimia 9.8 ya wanawake wanaotumia uzazi wa mpango hali ambayo imeongeza nguvu kubwa ya kuweza kuelimisha wanawake kuhusu huduma hiyo.

Changamoto,pamojana kwamba ndoa za utotoni zina athali kubwa sana  pamoja na kupoteza maisha ya watoto wa kike, sheria ya Ndoa ya mwaka 1971haiwalindi wasichana wenye umri wa miaka18 dhidi ya kuolewa, kwani sheri hiyo uwagusa wasichana wenye umri wa miak14 kuolew kwa ridhaa maalumu na maranyingi inaruhusu wasichana wenye umri wa miaka 15 kuolewa kwa ridhaa ya wazazi wao, Hali hii inaathiri maendeleo ya wasichanahisikana taifa kwa ujumla wanaharakati  wa masuala ya kijinsia na haki zabinadamuwamejitaidi kwa muda mrefu ili iweze kufanyiwa marekebisha bila mafanikio.
Ukeketaji,Pamoja na kuwepo kwa juhudi mbalimbali za kusitisha ukeketaji ikiwepo sheria inayozuia, hali halisi ya ukeketaji kwa watoto wa kike bado ni mbaya mkoa wa Mara kati ya mikoa 5 ya kitanzania ambayo inaongoza katika ukeketaji, Takwimu za afya za Taifa za mwaka 2010 zimedhihirisha kwamba asiloimia39 ya wanawakewamekeketwa.

Ukeketaji huo unaofanyika katika mikoa mbalimbali hapa Tanzainia ikijumuishaMara imechangia wanawake million tatu ambaoni sawana asilimia14.6 ya wanawakeawote nchini wote wamekeketwa.

Mwaka 2004 hali halisi ya ukeketaji mkoani Mara ilikuwa asilimia38.1 hatahivyo kufikia mwaka 2010 vitendo hivyo vimeongezeka hadi asilimia 39.9amabalo ni angezeko la asilimia1.8,ongezeko hilo linaonesha kuawa badojuhudi za serikali na mashirika kwa kushirikiana na jamii bado nindogo sana.

Toka kuanzishwa kwa TGNP Mtandao mwaka1993 wamekuwa mstari wa mbele katika kupigania haki na usawa wa motto wa kike ikiwa ni pamoja nakupinga vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia ikiwemo ukeketaji,

BadoTanzaniakumekuwepo na changamoto kubwa kwa vituo vya polisi na idara za ustawi wa jamii kutokuwa na mahala salama pa kuwahifadhi wahanga wa ukeketaji na hiyo kusababisha wasichana wengi ambao wameelimishwa na kuelewa madhara ya ukeketaji  kujiluta wanaburuzwa kwa nguvu  kupitaia vitendo hivyo.

                                

Powered by Blogger.