Asakwa kwa kubaka:

Asakwa kwa kubaka:

SIKU mbili baada ya Shirika la TGNP kuandaa tamasha la kupinga vitendo vya ukati,unyanyasaji,ndoa za utotoni na ukeketaji kwa watoto wakike vinavyo fanywa na baadhi ya watu wenyeuelewa mdogo Wilayani Tarime Mkoani Mara Binti wa Miaka kumi amedaiwa kubakwa  na kuumizwa vibaya katika viungo vyake na Kijana wa miaka 23.
 
Akielezea tukio hilo Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Motana Amosi Sameli alisema kuwa walikuwa katika kikao cha Katibu Tarafa Inano Marwa Lutha Ofisini kwake majira ya saa 6_7 mchana tarehe,03,07,2014 ambapo gafla walisikia yowe ikipigwa walipotaharuki walikuta watu wengi wakiwa wameandamana wakiwa na Binti huku  wakisema kuwa amekimbia mbakaji.
 
‘’Nilipo sikia kelele hizo ilinibidi nifuatilia kwa karibu ambapo kundi hilo la watu waliniambaia kuwa wamemkuta binti huyo akiwa anagaragazwa chini na kijana Nyitika Wiliphabosi 23 wa kijijini hapo kwa lengo la kutaka kumbaka ambapo kijana huyo amefanikiwa kutoroka  baada ya watu kuwa wamefika katika eneo la tukio’’alisema Samweli.
 
Samweli aliongeza kuwa alitoa ushauri kwa  wazazi wake kwenda kutoa taarifa kituoni polisi na kupewa PF3 kwa ajili ya kwenda hospitali kupata matibabu ambapo  mzazi wa kike wa binti huyo Mery Marwa Lutter 50 alifuata ushauri huo na kuchukua hatua ya kumpeleka kituoni polisi na kupata PF3.
 
Akitoa maelezo mbele ya mwaandishi wa habari hizi Mamam mzazi Mery wa binti huyo ambaye jina tunalihifadhi alisema kuwa Mbakaji alimdanganyishia kwenda kumpa nyama kwa ajili Mtoto kwa lengo la kwenda kupika  katika Mgahawa Mama ntilie kijijini hapo ambapo alifika njiani na kuanza kumlazimisha kuvua nguo ambapo binti huyo alikataa na kuanza  kulia huku akipiga  yowe ambapo  nilisikia na kutuka nje kijana huyo alipo ona hivyo alimwaacha na kuzunguka upande wa pili kumvizia tena njiani.
 
‘’Mara yapili alimfutaa tena akiwa anarudi kipandani kwa mamantilie ambapo alimkaba na kumchukua kinguvunguvu huku akiwa anamtishia hadi vichakani mbali kidogo na Nyumbani kama mita 300 ambapo aliazna kumvua nguo na kuanza kushiriki naye kwa nguvu kumlazimisha kuchukua hela ili asiseme ambapo nilisikia keleke nikatoka nikafuata zinakotokea ni kakuta ni binti yangu akiwa anabakwa na yuleyule kijana kwa mara ya pili’’aliongeza kusema Mama huyo.
Kwa upande wa    Msaidizi wa kisheria kituo cha manga Ayubu Gabriel alisema kuwa amesikitishwa na kitendo hicho na kuomba Serikali kutoa makucha kwa wale wote ambao wanabainika kufanya vitendo kama hivyo.
 
Aidha Gabriel alitoa rai kwa jeshi la polisi kuhakikisha kuwa mtuhumiwa wa tukio hilo  anakamatwa na kufikishwa katika sehemu husika na sheria kuchukua mkondon wake.
 
Tamwa ni chama cha waandishi wa habari wanawake wamekuwa mstari wa mbele kutetea haki za binadamu naye Mkurugenzi wa chama hicho Varelia Msoka alipopigiwa simu kuhusiana na tukio hilo alisema kuwa jamii isimamie ukweli na iweze
kujitokeza mahakamani kwa lengo la kupata haki zao za msingi.
 
Jamii ijijengee msimamamo wa kusimamia ukweli ilikuweza kutokomeza vitendo hivi vya kinyama alisema  Bi:Msoka
 
Hata  hivyo Bi Msoka amekeamea kitendo hicho cha kinyama na kutoa wito kwa jamii kuondokana na vitendo vya kinyama kwani vitendo hivyo vinawanyima watoto haki zao za msingi.
                           ……..Mwisho…
Powered by Blogger.