Nusuru shilingi elfu mbili imutoe roho binti mwenye umri wa miaka 18 wilayani Tarime mkoani Mara;

Picha ya binti aliyefanyiwa vitendo vya vya kikatili wilayani katika kijiji cha Murito  (Nyamongo) wilayani Tarime Mkoani Mara


Nusuru shilingi elfu mbili imutoe roho,

Binti mmoja aliyefaamika kwa jina la Agness  Marwa Chacha mwenye umri wa miaka 18 mkazi wa kijiji cha Murito kata ya kemambo(Nyamongo) wilayani Tarime mkoani Maraamenusurika  kuawa na mme wake aliyefaamoka kwa jina la Marwa chacha  kisyengi mkazi wa mrito mkulima.

Binti huyo alichomwa vikali sehemu za siri kwa kiginga cha moto na makalio yake na mmewe kwa kile kinachosemekana ni wivu wa kimapenzi ni baada ya mme wake binti kukuta shilingi elfu mbili katika pochi na kuanza kumushambulia kwa fimbo.

“Alipo fika nyumbani alinikuta na kuniuliza kuwa pesa iliyokuwa kwenye pochi imetoka wapi nakudai kuwa nimeongwa na wanaume wakati hiyopesa nilikuwa siijui ndipoa aliaanza kunipiga baadae kaniweka njee akanifunga nikanyeshewa mvua badae akatafuta kiginga cha mota akaanza kunichoma sehemu zangu za siri na makalio” alisema Agness.

Mganga mkuu katika hospitali ya sungu sungu Dr kagumilwa kaijage ambapo alilazwa mgonjwa huyo alisema kuwa binti huyo baada ya kuungunguza julai 13 mwaka huu hakuweza kuripoti hospitalini na badala yake  ariripoti  julai 17 mwaka huu na kuanza kuripotiwa akiwa ameaoaza sehemu za siri na mapaja.

“Tumempokea haspitali akiwa ameisha oza sehemu zake za siri zikitoa usaha na kuanza kutoa huduma”  alisema mganga mkuu.


Kwa mjibu wa maelezo ya docta binti huyo mbali na kufanyiwa vitendo hivyo vya ukatili ana mimba ya mwezi mmoja na nusu.

Kupitia mashirika mbali mbali ya kutetea haki za binadanu likiwemo chama cha waandishi wanawake Tamwa chini ya mkurugenzi wake varelie  msoka  wamekuwa mstari wa mbele kupigania haki ya mwanamke ikiwa ni pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia lakini jamii haiku tayari kubadilika.

Kulingana na nukuu iliandaliwa na chama hicho cha waandishi wa habari wanawake Tamwa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kama ilivyofanyiwa marekebisho ya mwaka 1977 na mwaka 2001 inatambua haki ya kila binadamu sasa inakuwaje jamii inakiuka sheria hii na serikali inakaa kimya japo mashirika yasiykuwa ya kiserikali yanazidi kulipigania kwa lengo la kureta mabadiliko  na kama ilivyo ibara ya 13:6(e) ya katiba inayosema ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa, kinyama au kupewa adhabu ya kudhalilishwa lakini vitendo hivi vimekuwa vikiendelea na serikali imekaa kimya.

Kwa upande wake mama mazazi wa binti huyo  Bi Nsato Marwa alikemea vikali kitendo hicho cha kinyama na kuiomba serikali kulivalia njuga ili mtuhumiwa kutiwa hatiani kwa ili liwe fundisho kwa jamii.

“Mwanangu ameharibiwa na mimi sina pesa za kumfanyia matibabu naomba msaada kwa Taasisi za serikali na zisizokuwa za kiserikali mashirika ili kuweza kunusuru mwanangu walikuwa wakimsaidia katitika matibabu wametoroka baada ya kusikia wanatafuitwa na jeshi la polisi” alisema mama mzazi.

Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi Tarime Rorya  kamishina msaidizi wa polisi Lazaro Benedict alidhibitisha kutokea kwa tukio hilo la kinyama na kusema kuwa na kuwataka jamii hiendelee kutoa taarifa mapema kwani taarifa hizo walizipata wakiwa wamechelewa.
                                                       ………Mwisho….





Powered by Blogger.