KAMPUNI ZA KUNUNUA TUMBAKU ZAOMBWA KUJA KUWEKEZA TARI



KAMPUNI ZA KUNUNUA TUMBAKU ZAOMBWA KUJA KUWEKEZA TARI
Tarime:
WADAU wa Tumbaku Wilayani Tarime Mkoani Mara wameomba makampuni mbalimbali yanayo nunua zao la tumbaku kujitokeza kuja kuwekeza Tarime ili kuwepo na ushindani wa bei ya kununulia badala ya kampuni ya ALLANCE ONE  iliyopo.

Wadau hao walisema hayo juzi,24,2014 Kwenye semina ya kuwajengea uwezo wadau wa tumbaku iliandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Tumbaku Tanzania (TORITA) juu ya Uandaaji na utunzaji sahihi wa vitalu(uwekaji wa pepete na mbolea).

Akizungumza Veronika Gabriel ambaye ni Ofisa Tumbaku wilayani Tarime kwa niaba ya wenzake alisema kuwa wakulima wa zao la tumbaku Wilayani Tarime wanapunjika wakati wa kuuza tumbaku kwa kampuni ya Allance One kuwa moja na kuwa kampuni hiyo haina mshindani hali ambayo inasababisha wananunua zao hilo kwa kujisikia.

''Kampuni ya Allance One unanunua Tumbaku kutoka kwa wakulima kwa kujisikia ambapo kwa kilo moja ya tumbaku watoa Tsh 350,badaya ya Tsh 3500 ambayo Kampuni ya Allance One ya Kenya inanunua kutoka kwa wakulima wakati wanapo peleka kuuza huko''alisema Veronika.

Aidha Veronika aliongeza kuwa kutokana ukosefu wa soko la uhakika wakulima wa Tumbaku wametishia kuchoma tumbaku likiwa shambani na kupanda mazao mengine ili kuondokana na usumbufu wanaoupata na pia kutorosha tumbaku kwenda Nchi jirani ya Kenya kunasababisha halmashauri kukoswa mapatoaliongeza kusema.

Kwa upande wake Afisa Mafunzo ambaye ametoka  taasisi ya utafiti  wa Tumbaku Cleophace Mathias alisema kuwa jukumu la kampuni iliyo kubaliwa kununua tumbaku kisheria inatakiwa kufuata taratibu  zilizopo pasipo kuzikiuka.

Aidha Mathias aliongeza kuwa uongozi wa Serikali unapaswa kusimamia taratibu zilizowekwa ili kuwasaidia wananchi wake na kuhakikisha kuwa makampuni yanalipa ushuru na pato la Taifa linaongeze na Wananchi wake wananufaika. 
                              ,,,,,mwisho…
Powered by Blogger.