Jamii yatakiwa kudumisha upendo,Amani na Mshikamano:



Jamii yatakiwa kudumisha upendo,Amani na Mshikamano:
 Tarime:
KANISA la Wadiventista Wasabato Mara Conference la Tarime kati limewataka waumini wa kanisa hilo kufanya kazi ya Uinjilisti  na kudumisha upendo kwa lengo la kuongoa Roho za Watu kwenda kwa Y esu ambao wanapotea  bila kumjua  mwenyezi Mungu.

Kauli hiyo imetolewa na Mzee wa kanisa hilo Alphonce Maigga jana wakati akihutubia Washiriki katika ibada ya  kuhamasisha siku ya changizo la harambee ambayo inatarajiwa kufanyika hapo September,09,2014 kwa ajili ya upanuzi na Ujenzi wa kanisa ili kukidhi mahitaji ya Kanisa.

Maigga alisema kuwa Kanisa ni chombo ambacho kiliundwa na Mungu mwenyewe kwa lengo la  kumwakilisha hapa Duniani na kuwa kufanya kazi ya uijnjilisti ni kufanya moja ya  kazi ambazo Bwana Yesu aliifanya hapa Duniani.

Aidha Maigga aliongeza kusema kuwa kazi ya Uinjilisti ni moja ya huduma takatifu ambayo Washiriki hawana budi kuitekeleza kama Bwana Yesu alivyo itekeleza alipokuwa hapa Duniani aidha aliongeza kuwa Watu wakimjua Mungu wataacha mabaya na Watamwekelea Mungu,wataacha mabaya na Wataishi kwa Amani na Upendo kama alivyo agiza Bwana  Yesu.

Wakili wa mali ya Bwana wa kanisa hilo Gregory Mbeba alisema kuwa lengo la kuaandaa harambee hiyo ni kutokana na Waumini kuzidi uwezo wa kanisa wa kuchukuan waumini 400 kwa sasa ambapo wamefikia waumini 2160 na swala ambalo linasababisha waumini wengine kusalia Nje ya kanisa huku wengine wakuwa ndani ya kanisa.

“Tunaomba  wadau wote wapenda maendeleo  kujitokeza kwa wingi kuja  kuchangia kanisa letu na watabarikiwa na Bwna Mungu na kufanya hivyo kutatusaidia  kukamilisha ndoto zetu za upanuzi na ukarabati wajengo la Kanisa ili kukidhi mahitaji ya Kanisa” alisema Mbeba.

Kanisa hilo limekisia kukusanya Tsh 100,000,000 katika harambee ambayo inatarajiwa kufanyika hapo September,09 mwaka huu na kuwa katika jitihada za kanisa hilo zimekwamakutokana na uwezo mdogo ambapo wameomba wadau kujitokeza na kutoa michango yao kkwa lengo la kufanikisha na kuondoa usumbufu uliopo.
            ………….....mwisho…………
Powered by Blogger.