Wananchi wataka shule kufunguliwa
Wakazi wa kijiji cha Tatwe, kata ya
Goribe, Wilayani Rorya, mkoani Mara, wameitaka serikali kufungua shule ya
msingi Nyanjogu kuwapunguzia adha watoto wa chekechea wanaosoma katika shule
hiyo kisha kwenda kuandikishwa katika shule ya msingi Tatwe iliyoko umbali wa
zaidi ya kilomita 10.
Wakazi hao walisema kuwa watoto wao
wanaotaka kitongoji cha
Nyanjogu hutembea mwendo mrefu kwenda kutafuta masomo katika shule ya msingi
Tatwe na wengine wakiugua na kulala njiani kutokana na umri wao.
Shule hiyo iliyojengwa kwa nguvu za
wananchi miaka mitatu iliyopita, ina vyumba viwili vya madarasa na ofisi
ya walimu lakini haijafunguliwa rasmi kutokana na kutotim iza matakwa ya
uongozi wa halmashauri kwa kufikisha vyumba vinne vinavyotakiwa na kukamilisha
ujenzi wa nyumba ya mwalimu ambayo iko kiwango cha kupauliwa.
“Watoto wakiugua wanalala njiani kwa
sababu ya mwendo mrefu wanaotembea na kwa kuwa wanachoka wanalala njiani, juzi
nilimkuta mtoto ameugua na kulala njiani baada ya kuzidiwa na kutembea kwa
mwendo mrefu kurudi nyumbani” alisema Jeshi Nyango mwenyekiti wa kijiji cha
Tatwe.
Hata hivyo Diwani wa kata ya Goribe Lucas
Ong’eto alisema kuwa kuchelewa kukamilika kwa shule hiyo kunatokana na viongozi
wa kisiasa kuingilia utekelezaji wa shughuli za maendeleo na kuusababisha kuwa
mgumu kwa kuwagomesha wananchi kutokana na utofauti wa kiitikadi.
“Nilienda halmashauri kuomba waje kufungua
shule ile nikaambiwa kuongeza vyumba viwili vya madarasa, choo cha
wanafunzi na kukamilisha nyumba ya mwalimu. Nilipoitisha wananchi kwenye
mkutano wa kuchangia maendeleo hawakuonekana nikakaamwenyewe tangu saa
nne asubuhi hadi saa 10 jioni nikarudi nyumbani bila mtu mmoja kuonekana”
alisema Ong’eto.
Mbunge wa jimbo la Rorya lameck
Airo aliliona suala hilo la watoto kuugua na kulala njiani kuwa ni zito
akaitaka kamati ya shule kesho yake juni 20 kufuata vifaa vya ujenzi ili
kukamilisha sehemu iliyobaki wanafunzi wanapofungua shule july saba waanze
masomo mara moja.
“Kwa kuwa mabati yanayohitajika
ni 46 kwa ajili ya kupaua nyumba ya mwalimu kesho mje mkachukue ofisini kwangu,
na mifuko 20 ya saruji ili kukazia sehemu iliyobaki. Na baada ya kukamilika
diwani uende kwa mkurugenzi mtendaji kumtaka aruhusu shule hiyo ifunguliwe
kuwanusuru watoto”alisema Airo.