Mwenyekiti wa kijiji atajwa kukumbatia wezi Rorya:



Mwenyekiti wa kijiji atajwa kukumbatia wezi
 Rorya:
Wanakijiji cha Kitembe kata ya kitembe Wilayani Rorya wameonyesha kutokuwa na imani na mwenyekiti wa kijiji hicho Andrew Odiwa wakimtuhumu kushirikiana na wezi katika kata ya Kitembe na kuiletea sifa mbaya Wilaya.

Walisema  kuwa Odiwa yeye  kama kiongozi waliyemwamini na kumchagua hashirikiani nao katika shughuli za maendeleo kijijini badala yake diwani ndiye huzifanya huku vikao vikiitishwa kwa ajili ya maendeleo yeye huitisha mgomo kwa baadhi ya wananchi akidai anazungumzia mambo ya chama.
Walisema hali hiyo imewafanya wamtilie shaka kuhusiana na nafasi aliyonayo kwao, kuwa haifai badala yake aondolewe ili kupisha mtu mwingine aishike  kwa muda wakati uchaguzi ukisubiriwa kufanyika.

Katika mkutano wa kata ulioitishwa na diwani wa kata  ya Kitembe Thomas Patrick ukishirikisha viongozi wa ofisi ya mkuu wa Wilaya, jeshi la Polisi mkoa wa Tarime Rorya kujadili Wizi na wezi wa mifugo katani humo ukifanyika kijiji chaKitembe, mwenyekiti wa kijiji hicho aliitisha kikao cha chama cha mapinduzi huku akipinga kufanyika kwa mkutano huo kijijini hapo.

Wananchi hao walisema wako tayari kukaa bila kuwa na kiongozi kwa kuwa miaka miwili iliyopita Odiwa alinusurika panga za wananchi baada kutajwa kuhusika kwenye wizi wa ng’ombe waliokuwa wakiibiwa kijijini hapo na kukimbilia kwa polisi kujinusuru.
“Kero yetu kubwa ni uongozi wa kijiji haututendei haki, mwenyekiti ni mpinzani wa maendeleo yetu wanakijiji, diwani anapoonyesha juhudi ya kuleta maendeleo, mwenyekiti anakuwa mpinzani wa kuyapinga, hata leo hali halisi imeonekana kwa kutokuwepo kwenye mkutano ulioshirikisha Mbunge kijijini kwake”alisema Lameck Nyang’era mkazi wa kitembe.

Hata hivyo mwenyekiti huyo amedaiwa kwenda kutoa ushahidi kwa polisi pale wezi wanapokamatwa na kufikishwa kituoni kuwa si wezi bali kilichofanyika ni fitina na wezi kuachiliwa kurudi kuwatishia wanaotoa ushahidi.
“viongozi tuliowachagua wanashirikiana na wahalifu kwa kupewa pesa ili wawatetee, mwenyekiti wa kijiji amekuwa akitoa ushahidi wa uongo polisi wa kuwatetea majambazi kuwa sio” alisema Charles Ongiro mkazi wa kitembe.

Diwani wa kata hiyo Thomas Patrick alito m wito kwa mkuu wa Wilaya na jeshi la polisi kusikia kilio cha wananchi wa kata ya kitembe wanapolia kuwa wanashida ili wasaidiwe pale wanapowambia kuwapo mwizi.

Patrick aliwatahadharisha wananchi hao kuwa ikiwa hawataona umhimu wa kudhibiti wezi kwa kuwataja waziwazi itafika wakati ambapo vijana wa kike na kiume wasipate pa kutembelea kutokana na sifa zao kuwa mbaya kwa wizi na ushirikina ulioko katani hapo.

“Itafika wakati hata mabinti zetu wataogopwa hata kuposwa kutokana na uchawi ulioko katani humo, kata yetu inasifika kwa wizi na uchawi, hii ni aibu kwetu wanakitembe,wachawi ninaowaomba muone aibu muachane na tabia hii chafu”alisema Patrick.

Diwani huyo aliongeza kuwa suala la Wizi wa Mifugo litamalizwa na wanakijiji wa kitembe  endapo wataunganisha nguvu ya pamoja na kuonesha ushirikiano wa pamoja .

Hata hivyo diwani huyo alizidi kukemea suala la Ushirikina ambalo linazidi kuendelea kijijini hapo kwa hivi karibuni kijana alipotea takribani siku tatu na kurejea siku ya tatu akiwa bubu
‘Jamani ondokana na Suala la Uchawi vijana ni wenu kwanini munawapoteza kwa njia zisizoeleweka tutafikia hatua tuwatengee wachawi wote’ alisema diwani.
Powered by Blogger.