VIKOBA OMBENI MIKOPO BENKI:


Mgeni rasmi Bw: Perdas Masungwa kulia kwake mwwenyekiti wa kikundi hicho Bi: Sophia Ahamed katika sherehe za kikundi cha tujijenge zilizofanyika jana katika ukumbi wa bwalo la polisi wuilayani Tarime mkoani Mara



Asasi za kuweka na kukopa (VICOBA ) zimeshauriwa kukopa mikopo katika banki mbalimbali kwa lengo la kutunisha mifuko yao ili kuweza kuendeleza  miradi mbalimbali waliyonayo.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Tarime Venance Mwamengo katika  kujibu taarifa ya utendaji kazi wa kikindi cha kuweka na kukopa Tujijenge VICOBA  katika ukumbi wa Bwaro la polisi Wilayani Tarime Mkoani Mara.
Mgeni rasmi huyo Bw:Pedas Masungwa kwa niaba ya mkurugenzi wa mji wa Tarime  alisema kuwaVicoba hivyo viweze kutuma Maandiko mbalimbali katika Taasisi kubwa za kifedha kwa lengo la kupata mikopo na kuweza kutunisha mifuko yao ili kuweza kukopesha wanachama hao fedha za kutosha.

“Tunazo taasisi nyingi za kifedha NMB, CRDB tumeni andiko ili muweze kukopeshwa fedha za kutosha kwa lengo la kupanua miradi mliyonayo pia wekeni miradi yenu  sehemu zenye ushindani mkubwa”  alisema mgeni rasmi.

 Mkufunzi wa VICOBA hivyo Bw : Emmanuel Buchafwe  katika kuwasilisha taarifa ya VICOBA kuanzia 04 julai Mawaka jana mpaka 29 juni Mwaka huu  alisema kuwa lengo la kuanzishwa kwa asasi hiyo kuinua  hali ya maisha kwa wanachama na familia zao kijamii, kiuchumi,kimazingira na kitamaduni ambapo kwa sasa tangu kuanza ni miaka mitano,  kikundi kwa sasa kina wanachama 30 wanawake 26 na wanaume 4 na walianza wakiwa wanachama 17 ongezeko la wanachama 17.

Hata hivyo mkufunzi huyo aliyataja mafanikio ya kikundi hicho kuwa wanacha wameweza kusomesha watoto, kuendeleza bihashara zao,kusaidia maafayanapotokea,wanachama kutumia rasilimali muda na fedha kwa kubuni na kuanzisha mradi wa mashine tatu mashine 2 za kusaga na 1 ya kukoboa ukiwa na thamani ya shilingi 8,3000,000fedha za kitanzania

Sanjari na hayo alizitaja changamotozinazowakabili kuwa ni Wanachama kutorejesha mikopo kwa wakati,kutozingatia katiba ya kikundi hicho,jamii kutojua umuhimu wa mfano jinsi unavyosaidia jamii yenye kipatocha chini,na wanachama kutoweka staid za maarifa,mbinukatika kusimamia miradi ya kiuchumi.

Wameitaja  mikakati waliyonayo kuongeza miradi ya kiuchumitoka asilimia30%ya sasa hadi kufikia asilimia 60%, kuboresha ukopeshaji wa kwa kupunguza nyongeza na bimatoka asilimia15%ya2013 hadi asilimia10 ya 2014-2015 pamoja na kununua kwa mashine yenye uwezo wa kusaga, kukoboa,kupimakupakia na kushona mifuko uku wakitoa changizo la shilingi kwa lengo la kutunisha mifuko yao.

Wanachama hao wa Tujijenge VICOBA wameomba Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Tarime kuwapa eneo kwa lengo la kujenga ofisi zao ili kuweza kufanyakazi kwa ufanisi.

                                     ……….Mwisho…….

Powered by Blogger.