Vijana watakiwa kumrudia Mwenyezi mungu:



Vijana watakiwa kumrudia Mwenyezi mungu:
Rorya.
Vijana Wilayani Rorya mkoani Mara wametakiwa kumrudia mwenyezi mungu ikiwani pamoja na  kuondokana na suala la wizi wa mifugo ambao umekuwa kero wilayani humo.

Kauli hiyo imetolewa na mbunge  wa jimbo la Rorya Bw:Lameck Airo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha utegi wilayani humo, kwa lengo la kuzungumzia mgogoro wa ardhi kati ya Umoja wa vijiji sita vinavyozunguka ardhi hiyo (UMONI)  mwekezaji wa  kampuni ya(UDAFCO)chini ya usimamizi wa mkurugenzi wake Otieno Igogo.

Lameck alisema kuwa vijana waliowengi wamekuwawakijiusisha katika suala la wizi wamifugo na uku wengine wakiusika kukaribisha waharifu kutoka wilaya jirani na kuiba mifugo hiyo.

“Kijiji cha Utegi kuna kijana mmoja na Nyanduga kuna vijana wawili natoa agizo kwa serikali za vijiji kuitisha mikutana ili niweze kuleta kijana mmoja ambaye amejisalimisha na kuanza kuwataja wezi ili wakamatwe” alisema Lameck.

Aliongeza kuwaendapo vijana hao watamtumikia mwenyezi mungu itasaidia kuwabadili tabia na kuondokana na suala la wizi wa mifugo kwani limewanyima amani wakazi wa Rorya na Vijiji vyake.

Aidha mbungea huyo alisema kuwa asilimia kubwa ya wakazi wa rorya ni wafugaji hivyo mifugo hiyo utumika kuwasomesha watoto endapo wizi utaendelea watoto hawanda shule kwani kipato kinapungua kutokana na wizi huo.

Sanjari na hayo kutokana na Mgogoro wa ardhi ambao umekuwepo takribani miaka kumi na tatu kati ya wananchi na mwekezaji ameamua kuzunguka katika vijiji sita kwa lengo la kukusanya maoni ya wananchi uku wakipiga kura za wazi ili waweze kuwasilisha maoni hayo kwa waziri mwenye dhamana kwa lengo la kutatua mgogoro huo.

“Tumemaliza mzunguko wa vijiji vyote  tumepata maoni ya wananchi wanaoteseka tunaenda kuyafanyia kazi  asilimia kubwa kulingana na takwimu tuliyopata kutoka kwa wananchi na  wamedai kurudishiwa ardhi yao ili waweze kulima au kuleta mwekezaji mwinginea ambaye atawanufaisha” alisema Mbunge.


Powered by Blogger.