JAMII YA KIKURYA YAIMIZWAKUSOMESHA WATOTO ILI KUPATA FURSA ZILIZOPO NDANI YA WILAYA

Picha ya Mgeni rasmi Katibu Tarafa wa Inano Bw: Marwa Chaha kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele akitoa hotuba yake katika Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kiwila katika kata ya Muriba Tarafa ya Ingwe uku kauli mbiu ikisema kuwa kupata Elimu bora na Isiyo na Vikwazo ni haki ya kila Mtoto


Jamii ya kikurya imeimizwa kusomesha watoto kwa lengo la kuweza kupata ajila kupit ia  fursa zilizopo katika katika wilaya ya Tarime ususani mgodi wa dhahabu uliopo Nyamongo wilayani humo.
Kauli hiyo imetolewa na Mgeni rasmi katibu Tarafa wa Inano BW:Marwa Chacha  kwa niabaya ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika iliyofanyika kiwilaya katika  kata ya Muriba Tarafa ya Ingwe Wilayani humo, uku kaulimbiu ikisema kuwa Kupata Elimu bora na Isiyo na Vikwazo ni haki ya kila Mtoto.
Mgeni rasmi alisisitiza suala zimala Wazazi Walezi kuwekeza katika  suala zima la Elimu ili Watoto wawezekuondokana na  uvamizi wa mara kwa mara katika Mgodi wa North Mara na kupelekea baadhi ya watoto koteza Maisha yao na wengine kuwaVilema wa kudumu  kwa kupigwa Risasi katika Mapambano baina ya Jeshi la Polisi.
Alieleza kuwa suala zima la kushuka kwa Elimu na kutoroka kwa wanafunzi na kuacha shule na kujiingiza katika suala la  uvamizi wa mgodi ni mwamko mdogo wa wazazi na walezi katika Elimu.
“Wazazi tuungane kwapamoja kupambana na Ukatili dhidi ya Mtoto kumpa haki yake ya kupata elimu na kila mmoja wetu kutimiza wajibu wake ikiwa ni pamoja na kuondokana na kuozesha watoto mambo hayo yamepitwa na wakati” alisema Mgeni rasmi.
Hata hivyo Mgeni rasmi aliongeza kuwa kupitia Serikali wameunda mikakati mizuri ya kuanzishwa kwa vikundi vya ulinzi shirikishi kupitia jamii inayozunguka  mgodi huo ili kuweza kupunguza Mauaji  yanayotokea katika Mgodi huo ikiwa ni moja ya  kupatikana kwa ajila kwa  vijana hao.
Katika maadhimisho hayo Ofisa Maendeleo Bw Charles Ouma kwa niaba ya Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Tarime Bi:Dorotty Jovin amezitaja Takwimu zinazomugusa mtoto katika suala zima la Ukatili kuwa katika Mei mpaka juni Ndoa za utotoni zimeripotiwa 2 Mimba7 Ubakaji11 kurawiti1 shambulio kwa watoto7, utoroshaji wanafunzi 39 nakusema kuwa jumla yameripotiwa matukio 69 katika ofisi ya Ustawi wa jamii nakuitaka jamii kutoa taarifa pale matukio yanapojitokeza.
Katika kusoma Risala mbele ya Mgeni rasmi watoto hao  katika kupigania haki yao wamezitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni kubaguliwa kwa watoto wa kike katikafamilia ikiwa ni pamoja na kunyimwa haki ya kupata  Elimu wazazi uwaozesha watoto hao ili kupata kipato, kushawishiwa katika suala zima la  Ukeketaji suala ambalo ni hatari kwa afya,kuzidi kuongezeka kwa matukio ya kikatili dhidi ya mtoto wa kiafrika kupitia wazazi na walezi wao.
“Wazazi unganisha nguvu ya pamoja ili kutokomeza vitendo vya kikatili ikiwa ni pamoja kutoa kipaumbele na wekeza katika suala zima la Elimu na si kufikiria na kuwaza Mali za kutuozesha bali tuozeshe katika Elimu” walisema Watoto hao.
Hata hivyo kupitia  Maadhimisho hayo watoto hao wameiomba serikali kuangalia haki za mtoto na kumpa kipaumbele kwa lengo la kujikomboa, kupinga ili kukmesha suala zima la ukeketaji, kukomesha ajila za watoto na kuodheshwa katika umri mdogo.
Sanajari na hayo jamii imeimizwa kuanzisha suala zima la Mapambano katika kupinga ukatili wa Mtoto kuanzia katika ngazi ya kaya,ili kuweza kutokomeza  suala zima la Ukatili dhidi ya Mtoto, ikiwa ni pamoja na kuondokana na Uvamizi wa Mugodi wa African Barrick Golg ABG North Mara.
Kwa upande wake ofisa Ushirikishwaji kutoka katika Mgodi wa African Barrick Gold ABG Bw: Nikodemus Keraryo alisema kuwa Mgodi huo kwa kutambua  umuhimu wa Mtoto wanazidi kutekeleza miradi ya jamii kama vile ujenzi wa Shule,Zahanati.Barabara na huduma  nyingine.
“Tunatambua Umuhimu wa watoto hivyo tutazidi kusaidia jamii kupitia idara ya Mahusiano” alisema Keraryo.
Aidha Mgodi huo ili kuongeza hamasa katika suala zima la Elimu wamesema kua katika Wiki mbili mbeleni wataweza kupita katika shule 16 za Msingi zilizomo katika Vijiji  vinavyozunguka Mgodi huo na kutoa zawadi mbalimbali kwa watoto waliofauru vizuri Mwaka huu na kuomba na mgeni rasmi kuwa endapo wataanza zoezi hilo wahusishe viongozi wa serikali wakiwermo Maofisa Elimu  kwa lengo la kukutana na Wazazi ili kuzungumzia chanagamoto katika suala zima Elimu  hiyo.
                          …………Mwisho….
Powered by Blogger.