African Barrick Gold (ABG) ITAZIDI KUSAIDIA JAMII:

Ofisa Ushirikishwaji Bw:Nicodemus Keraryo akitoa shukrani zake kwa niaba ya Mgdi wa African Barrick Gold (ABG) katika Maadhimisho ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika ngazi ya Wilaya  katika Kata ya Muriba Tarafa Ingwe:



 Ofisa Ushirikishwaji kutoka katika Mgodi wa African Barrick Gold ABG Bw: Nicodemus Keraryo alisema kuwa Mgodi huo kwa kutambua  umuhimu wa Mtoto wanazidi kutekeleza miradi ya jamii kama vile ujenzi wa Shule,Zahanati.Barabara na huduma  nyingine.

“Tunatambua Umuhimu wa watoto hivyo tutazidi kusaidia jamii kupitia idara ya Mahusiano” alisema Keraryo.

Aidha Mgodi huo ili kuongeza hamasa katika suala zima la Elimu wamesema kua katika Wiki mbili mbeleni wataweza kupita katika shule 16 za Msingi zilizomo katika Vijiji  vinavyozunguka Mgodi huo na kutoa zawadi mbalimbali kwa watoto waliofauru vizuri Mwaka huu na kuomba na mgeni rasmi kuwa endapo wataanza zoezi hilo wahusishe viongozi wa serikali wakiwermo Maofisa Elimu  kwa lengo la kukutana na Wazazi ili kuzungumzia chanagamoto katika suala zima Elimu  hiyo.
                        

 

Powered by Blogger.