DC TARIME AKEMEA SUALA LA UVAMIZI WA MGODI:


Katibu tarafa wa Inano Bw:Marwa Chacha kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele amekemea suala la Vijana kuvamia Mgodi wa dhahabu wa African Barrick Gold ABG North Mara, suala ambalo linasababisha kupoteza kwa Maisha ya  vijana hao baada ya kupata Dhahabu hizo baadhi upelekea kuuana wakati wakinuyanganyana dhahabu hizo uku wengine wakipigwa risasi na Jeshi la Polisi wakati wa kupambana kipindi wakifukuzwa  kutoka ndani ya Mgodi huo nakupelekea kupoteza maisha na wengine kuwa vilema wa kudumu.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni mbele ya Wazazi na Walezi katika Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kiwilaya katika kata ya Muriba Tarafa ya Ingwe,uku kaulimbiu ikisema kuwa Kupata Elimu bora na Isiyo na Vikwazo ni haki ya kila Mtoto.
Aidha Mgeni rasmi alisisitiza wazazi kuwapatia Watoto wao Elimu ili waweze kuajiliwa ndani ya Mgodini huo baada ya kupata sifa za kuajiliwa nasikutumia nguvu katika uvamia Mgodi huo.
“Mgodi siyo Mali ya Mzungu ni Mali ya Serikali kwa sababu wanalipia kodi endelea kuhamasisha vijana wenu waondokane na kuvamia Mgodi na wekezeni kwenye Elimu ili kunusuru vijana hao na  suala la uvamizi  litapungua” alisema.
Hata hivyo Mgeni rasmi aliongeza kuwa wamejipanga kugawa maeneo ya wazi kwa lengola kuwanufaisha Wachimbaji wadogo ili kuweza kupunguza suala la Uvamizi wa Mara kwa Mara ambao ni Changamoto kubwa.
Vilevile mgeni rasmi aliwataka wazazi na walezi kutoa ripoti katika vyombo vya dola pale vitendo vya ukatili vinavyotokea ili kukomesha ukatili dhidi ya Watoto.
“Ofisi ziko wazi madawati ya jinsia yapo na jeshi la polisi linafanya kazi vizuri toeni tarifa ili waharifu wachukuliwe hatua mara moja” alisma Mgeni rasmi.
Kwa upande wake ofisa Ushirikishwaji kutoka katika Mgodi wa African Barrick Gold ABG Bw: Nikodemus Keraryo alisema kuwa Mgodi huo kwa kutambua  umuhimu wa Mtoto wanazidi kutekeleza miradi ya jamii kama vile ujenzi wa Shule,Zahanati.Barabara na huduma  nyingine ili mtoto wa Afrika aweze kupata haki yake ya Msingi hususani Elimu.
“Tunatambua Umuhimu wa watoto hivyo tutazidi kusaidia jamii kupitia idara ya Mahusiano” alisema Keraryo.
Aidha Mgodi huo ilikuongeza hamasa katika suala zima la Elimu mbele ya Mgeni rasmiwalisema kuwa  katika Wiki mbili mbeleni wataweza kupita kila  shule kati ya shule 16 za Msingi zilizomo katika Vijiji  vinavyozunguka Mgodi huo na kutoa zawadi mbalimbali kwa watoto waliofauru vizuri Mwaka huu na ndipo Mgeni rasmia aliwataka viongozi wa Mgodi huokuwa   rasmi endapo wataanza zoezi hilo wahusishe viongozi wa serikali wakiwemo Maofisa Elimu  kwa lengo la kukutana na Wazazi ili kuzungumzia changamoto  zilizopo katika shule hizo.
           
Powered by Blogger.