Rais Magufuli:Kilimo Kifanyiwe Mageuzi Ya Uchumi

Na Judith Mhina-MAELEZO
Mahitaji ya Soko la chakula Barani Afrika kwa sasa ni Bilioni 300 na Ifikapo mwaka 2030 itakuwa Trilioni moja.

Hayo yamesemwa na  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli wakati akizindua Mpango wa Programu ya Sekta ya Kilimo ASDP 11 jana  jijini Dar-Es-Salaam katika ukumbi wa Kimataifa Mwalimu Julius Nyerere Conventional Centre.

Rais Magufuli alisema nchi yetu ni kati ya nchi zenye bahati ya kuwa na ardhi ya kutosha ya uzalishaji kwa njia ya umwagiliaji kwa kuwa tuna vyanzo vingi vya maji. Hivyo ni lazima wakulima wetu  kunufaike na fursa hii ya kipekee iliyopo Barani  Afrika.

Akizitaja changamoto ambazo zikipatiwa ufumbuzi kutakuwa na mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo Rais Magufuli amesema “Kilimo lazima kiwe na tija ambapo eneo dogo la kilimo linakuwa na uzalishaji mkubwa”.

Akitoa njia za kufanya mageuzi hayo ya kilimo Rais ameongeza wakati umefika vituo vyetu vya Utafiti vya Kilimo, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine – SUA  kuhakikisha wanafanya tafiti zinazolenga kuongeza jita katika mazao yetu,

Aidha, Maafisa Ugani waache tabia ya kukaa ofisini, waende kwa wakulima na kuwashauri njia bora na sahihi zilizotokana na tafiti hizo ili Kuongeza uzalishaji maradufu na kuchochea uchumi wetu kukua kwa kasi.

Amewaasa watendaji wa sekta ya kilimo kuwa na matumizi mazuri ya fedha za programu ambapo fedha zinazohitajika ni takribani shilingi za Tanzania Trilioni 13.82 kati ya hizo Serikali na Washirika wa Maendeleo watatoa asilimia 40 na Sekta Binafsi asilimia 60.

Rais Magufuli ameagiza na kusema haiwezekani nchi za wahisani na wafadhili mbalimbali watoe fedha zao, alafu utekelezaji wa program uwe hauridhishi kwa kutenga fedha nyingi katika shughuli za utawala badala ya kuelekezwa kwa walengwa.

“Programu ni lazima itafute muarobaini wa masoko ya mazao ya kilimo mifugo na uvuvi , hii ni pamoja na uwanzishwaji wa viwanda mbalimbali ambapo itachochea zaidi wakulima kuzalisha kwa wingi na kuondoa adha ya kutafuta masoko na kuwatia wakulima hasara” alisema Rais.

Akisisitiza jambo hili Rais Magufuli amewaagiza Mabalozi wote walioko nje ya nchi kuhakikisha wanatafuta masoko ya mazao mbalimbali katika nchi walizopo. Hii ni mojawapo ya majukumu yao katika sehamu zao za kazi

Serikali imefanya na inaendelea kufanya mazingira wezeshi ya kuhakkikisha mazao yanatoka vijijini kwa urahisi kwa kujenga miundombinu ya barabara na uwekaji wa umeme ili kuweza kuchakata mazao hukohuko katika sehemu za uzalishaji na kuziongezea dhamani.

Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi kuhakikisha inawekeza zaidi katika kilimo na viwanda vitokanavyo na mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi. Sekta binafsi ijipange na kuonyesha kwa namna gani itashiriki katika kilimo, viwanda na kufanya tafiti  zenyemanufaa katika kilimo.  

Aidha Rais Magufuli amenyooshea mkono na kuonyesha masikitiko yake kwa Benki ya Kilimo Tanzania TAB kwa kushiriki kutowapa mikopo na kuwatenga wakulima ambao ndio walengwa, na kutoa mikopo kwa watu wasiohusika wakiwemo watumishi wa Benki hiyo na wafanyabiasgara wengine. 

Malengo makuu ya Benki hiyo ni kutoa mikopo kwa wakulima wa mazaom wafugali wavuvi na makundi yote yanayojihusiha  na kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo.

Naye Waziri wa Kilimo na Ushirika Mhandisi Charles Tizeba amesema Programu ya ASDP 11, inakusudia kuongeza eneo la uzalishaji kwa njia ya umwagiliaji kutoka hekta 450 elfu  za awali hadi kufikia milioni 1.

Aidha, akionyesha baadhi ya Taasisi zilizofanikiwa kuzalisha kwa tija Tizeba amesema ”Taasisi ya Clintoni imefanikiwa kuzalisha kwa tija katika shamba la mahindi la hekari moja na kuvuna magunia 1500 kule Mkoani Iringa”.

Akitoa vipaumbele vya utekelezaji wa ASDP 11 ni pamoja na usimamizi wa rasilimali maji na matumizi ya umwagiliaji , ikiwa ni pamoja na kujiandaa kuzalisha kwa tija hata kama kunatokea mafuriko na ukame.

Kuongeza dhamani ya mazao kwa kushirikisha kikamilifu sekta binafsi, kuweka mazingira wezeshi katika sekta kwa kuondoa tozo 98 , kuwa na Sera zinazotabirikaili kukuza uchumi na kukuza pato la kilimo kutoka asilimia 3.7 hadi kufikia 6 kwa mwaka.

Akiongea kwa niaba ya nchi wahisani katika Sekta ya Kilimo  Mwenyekiti  Fred Kafeero amesema “ Nchi, Mashirika ya Kimataifa na Taasisi  zinazochangia katika programu ya ASDP 11 ni pamoja na Ubelijiji, Uingereza Jumuia ya Ulaya Ubalozi wa Denmark, Ufaransa, Uswiss, Canada,  Uholanzi, Bill and Melinda Foundation,  Benki ya Maendeleo Afrikam, Shirika la Maendeleo la Ujerumani,  Ireland,  AGRA, IFAD UNDP. UNIDO, USAID Benki ya Dunia.   
Powered by Blogger.