Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kuhamia vijijini sasa

Madiwani
wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara wakiwa katika baraza la
madiwani la kawaida ambapo kwa pamoja wote wameazimia kuhamia katika
Makao makuu ya Wilaya ambayo yatajengwa  Kijiji cha Nyamwaka kata ya
Nyamwaga ili kusogezea wanachi maendeleo ambapo wanachi wa kijiji cha
Nyamwaga wametoa hekari 128 bure bila kudai fidia.

Kushoto
ni Makamu Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Bathromeo Machage
katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Moses Misiwa Yomami na
anayefuatia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Tarime Vijijini Apoo Castro
Tindwa.
Madiwani wanapitia taarifa.
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Moses Misiwa Yomami ambaye pia ni
diwani wa kata ya Nyamwaga akisisitiza jambo katikabaraza la Madiwani
pia amemwomba mkurugenzi kukutana na watu wa ardhi ili wakutane na
kamati ya ulinzi na usalama kwa lengo la kuzungumzia masuala ya migogoro
ya ardhi katika vijiji..

Makamu
Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Bathromeo Machage
akisisitiza jambo katika Baraza la Madiwani ambapo alisema kuwa kuna
haja kubwa ya madiwani kukaa kwa pamoja ili kutatua suala zila la
Migogoro ya ardhi.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Apoo Castro Tindwa akisoma taarifa
katika Baraza la Madiwani likiwemo suala la kuhamia Makao mapya ili
kufikisjha huduma za wananchi karibu.

TAZAMA VIDEO MWENYEKITI MOSES NA MKURUGENZI WAKIZUNGUMZIA SUALA LA KUHAMIA NYAMWAGA MAKAO MAKUU YA WILAYA.

Powered by Blogger.