Breaking News " DAVID KAFULILA NAYE AJIONDOA CHADEMA


Mwanasiasa maarufu wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini.Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila leo ametangaza kujivua uwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kwa kile alichosema hana imani na vyama vya upinzani kama jukwaa salama la kupambana na ufisadi nchini Tanzania. 
Kafulila amejiondoa CHADEMA na baada ya maamuzi hayo ameeleza sababu kwamba kwa sasa vyama vya upinzani vinaonekana kupigwa ganzi na kupooza katika juhudi zake za kupambana na ufisadi na ghafla ufisadi sio agenda kuu tena ya vyama vya upinzani tena.
“Kwa kuwa sina imani tena na upinzani kama jukwaa salama la kupambana na ufisadi, nimeamua kwa hiari na utashi wangu kujivua uanachama wa CHADEMA kuanzia tarehe ya taarifa hii, nitatangaza kwa siku za hivi karibuni jukwaa jipya la harakati zangu dhidi ya ufisadi”- Kafulila


Powered by Blogger.