Angalia picha : MAHAFALI YA 9 KIDATO CHA NNE KOM SEKONDARI MWAKA 2017


Shule ya Sekondari Kom iliyopo mjini Shinyanga leo Jumamosi Novemba 11,2017 imefanya mahafali ya 9 ya kidato cha nne tangu kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2006.

Mgeni rasmi katika mahafali ya tisa ya kidato cha nne mwaka 2017 yaliyohudhuriwa na wazazi na wageni mbalimbali alikuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro.

Akizungumza katika mahafali hayo,mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro alisema mabadiliko yoyote yanaletwa na ushirikiano hivyo kupitia ushirikiano
Mkuu huyo wa wilaya alisema shule hiyo imekuwa maarufu kutokana na elimu bora inayotoa na kutokana na hali shule imeupatia sifa mkoa wa Shinyanga.

“Sisi kama serikali tunajivunia uwepo wa shule hii katika mazingira yetu kwani inatutangaza ndiyo, tupo tayari kushirikiana katika kutatua changamoto zinazojitokeza ili kusukuma gurudumu la maendeleo”,alieleza Matiro.

“Tupo tayari kuhakikisha kuwa tunashirikiana na sekta binafsi na milango yetu ipo wazi na panapotokea changamoto msisite kutufikia”,alisema.

Alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wazazi kuwekeza kwenye elimu kwa watoto kwani huo ndiyo urithi wenye thamani katika maisha yao.

Katika hatua nyingine aliipongeza shule hiyo kuajiri watu 63 katika shule kwani hiyo ni sehemu ya kuunga mkono lengo la serikali la kuzalisha ajira kwa wananchi.

Matiro aliwataka wanafunzi waliohitimu kidato cha nne kuwa mfano katika maeneo wanakokwenda na kuhakikisha matendo yao yanaendana na mambo waliyofundishwa shuleni.

Mkuu huyo pia aliupongeza uongozi wa shule kwa kuanzisha shule ya awali na msingi na hiyo inatokana na ushirikiano uliopo kati ya shule na wazazi ambao wamekuwa mstari wa mbele kusukuma maendeleo ya shule.

Naye Mkurugenzi wa shule ya Kom Sekondari Jackton Koyi aliishukuru serikali kwa ushirikiano ambao imekuwa ikiwapa katika kuhakikisha kuwa shule hiyo inafikia malengo yake.

Alisema Kom sekondari shule hiyo imetimiza miaka 12 tangu kuanzishwa kwake na imekuwa daraja la elimu kwa wanafunzi ambao wengi wamekuwa wakiingia kidato cha tano na kujiunga katika vyuo mbalimbali.

“Shule yetu imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani,mfano kati ya wanafunzi 160 waliomaliza kidato cha nne mwaka 2015,145 walijiunga na masomo ya kidato cha tano,na mwaka 2016 kati ya wanafunzi 144 waliofanya mtihani wa kidato cha nne,133 walijiunga kidato cha tano”,aliongeza Koyi.

“Naomba wazazi muendelee kutuamini na kuleta wanafunzi katika shule hii ambayo imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani mbalimbali”,alieleza Koyi.

Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo,Mwita Warioba alisema shule hiyo hivi sasa ina jumla ya wanafunzi 542,walimu 32 huku akisisitiza kuwa lengo la shule hiyo ni kutoa elimu bora.

“Shule yetu ina miundo mbinu ya kutosha,madarasa yapo ya kutosha,tuna umeme wa Tanesco,maji kutoka ziwa Victoria,mabweni 8,viwanja vya michezo,maktaba moja,maabara mbili ikiwemo ya Computer”,aliongeza Waryoba.

Awali akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wa kidato cha nne,Jackline Benson alisema walianza kidato cha kwanza wakiwa 104,ambapo wavulana walikuwa 52 na wasichana 52 lakini idadi iliongezeka na hivyo idadi ya waliohitimu kidato cha nne mwaka huu ni 154,kati yao wasichana ni 73 na wavulana 81.

Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde ametusogezea picha za matukio angalia hapa chini

Wahitimu wa kidato cha nne mwaka 2017 katika shule ya sekondari Kom wakimpokea mgeni rasmi katika mahafali ya tisa ya shule hiyo,mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro

Mkurugenzi wa shule ya sekondari Kom,Jackton Koyi akimpokea mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kwa ajili ya kushiriki mahafali ya kidato cha nne katika shule hiyo

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwapungia mkono wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kom

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya mkurugenzi wa shule ya sekondari Kom

Mwanafunzi wa kidato cha tatu Zena Ali akimweleza Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro historia ya shule ya sekondari Kom wakati wa maonesho ya shughuli mbalimbali zinazofanyika katika shule hiyo

Wanafunzi wa shule ya sekondari Kom wakionesha ramani ya dunia kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro

Mwanafunzi wa kidato cha tatu Rajuu Masudi akieleza kuhusu sanaa ya uchoraji inayofanywa na wanafunzi wa shule ya sekondari Kom


Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kom,Safia Ali akitoa maelezo kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro wakati wa maonesho ya kitaaluma

Kijana wa skauti akimvalisha skafu mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro wakati wanafunzi waliohitimu kidato cha nne wakiandamana kuelekea kwenye ukumbi wa sherehe ya mahafali hayo

Wahitimu wa kidato cha nne 2017 katika shule ya sekondari Kom wakiandamana

            Wahitimu wakiandamana

Mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikata utepe wakati wa mahafali ya tisa ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Kom.Kulia ni mwenyekiti wa bodi ya shule Peter Kugulu,kushoto ni mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom,Jackton Koyi

Wahitimu wakiingia ukumbini

Meza kuu wakipokea maandamano ya wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kom

Mkuu wa shule ya sekondari Kom,Mwita Waryoba akizungumza wakati wa mahafali hayo

Mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom,Jackton Koyi akizungumza wakati wa mahafali ya tisa ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Kom

Mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom,Jackton Koyi akizungumza

Wahitimu wa kidato cha nne wakiwa ukumbini

                               Wazazi wakiwa ukumbini

Wahitimu wa kidato cha nne wakipunga mkono

                            Wahitimu wakiwa ukumbini

                                Wahitimu wakiwa ukumbini

                    Wazazi wakiwa kwenye mahafali

Wahitimu wa kidato cha nne,Scholastica Simon na Dickson Nyansika wakikata keki wakati wa mahafali ya kidato cha nne mwaka 2017

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akimlisha keki mhitimu wa kidato cha nne Dickson Nyansika

Scholastica Simon na Dickson Nyansika wakimlisha keki mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro

Dickson Nyansika akimlisha keki Mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom,Jackton Koyi

                      Wazazi wakiwa katika mahafali hayo

Wazazi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea

                                Wazazi wakiwa eneo la tukio

                                      Mzazi akifurahia jambo

                                        Mahafali yanaendelea

                                Mahafali yanaendelea

Mkurugenzi wa shule ya Sekondari Kom (kushoto) ,Jackton Koyi na mke wake Magreth Jackton Koyi (kulia),wakipokea zawadi ya keki iliyoandaliwa na wazazi ,Ibrahim Okero na Lucia Ibrahim Okero (katikati) kwa ajili ya viongozi wa shule ya sekondari Kom

                        Wazazi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea

Baadhi ya wanafunzi wanaobaki katika shule hiyo wakiwa kwenye mahafali hayo

Wahitimu wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Kom wakiimba wimbo

Wahitimu wa kidato cha nne, Jackline Benson na Kelvin wakisoma risala

                       Vijana wa skauti wakitoa burudani

Mwanafunzi aliyejulikana kwa jina la Samwel akitoa burudani ya wimbo

Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari Kom Peter Kuguru akizungumza katika mahafali hayo

                       Wanafunzi wakionesha ubunifu wa mavazi

Wanafunzi wakiwa wamevaa mavazi mbalimbali ya ubunifu

                         Wanafunzi wakiimba shairi

Mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mahafali ya 9 ya kidato cha nne katika shule ya sekondari Kom

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mahafali hayo

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza

Wageni waalikwa wakiwa katika mahafali hayo


                                     Ma Dj wakiwa eneo la tukio

Mgeni rasmi Josephine Matiro akizungumza wakati wa harambee ya kuchangia kupatikana kwa samani katika bweni la wasichana katika shule ya sekondari Kom ambapo shilingi milioni 9 zinahitajika

Akina mama wakiwa katika foleni kwenda kuchangia fedha kwa ajili ya samani za ndani katika bweni la wanafunzi

                                               Harambee inaendelea

Akina baba wakiwa katika foleni kuchangia fedha kwa ajili ya samani katika bweni la wanafunzi

                            Harambee inaendelea

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga akishikana mkono na wageni waalikwa wakati wa harambee hiyo

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akitoa zawadi ya fedha kwa mmoja wa walimu katika shule ya sekondari Kom

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akitoa vyeti kwa wahitimu

                          Zoezi la kugawa vyeti likiendelea

              Wahitimu wakiwa katika foleni kupokea vyeti

Wahitimu wakijiandaa kupokea vyeti ya kuhitimu kidato cha nne.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Powered by Blogger.