BAKWATA wataka anayejiitwa Mtume akamatwe
Baraza
la ulamaa limetoa wito kwa vyombo vya dola kumchukulia hatua stahiki
mtu aliyejitokeza katika Mkoa wa Pwani na kudai yeye ni Mtume.
Akizungumza
jana na waandishi wa habari kwa niaba ya Mufti wa Tanzania, Sheikh
Abubakar Zubeir Ally, Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu Bakwata, Sheikh
Hamisi Said Mataka alisema, anachodai mtu huyo anayefahamika kwa jina
la Hamza Issa kuwa yeye ni Mtume ni kitu ambacho hakipo kabisa katika
mafundisho ya kiislamu.
Alisema
kauli ya Issa kudai yeye ni mtume na kisha kwamba ni muislamu na
kutumia maandiko ya uislamu ni upotoshaji mkubwa ambao ukiachwa bila
kudhibitiwa ni kuruhusu fujo na uvunjifu wa amani.
“Kwa
mujibu wa maelezo yaliyoenea katika mitandao ya kijamii na ya kutoka
baraza za Masheikh wa Mkoa wa Pwani chini ya kiongozi wake Sheikh na
Qadhi wa Mkoa wa Pwani, amedai kuwa yeye ni Nabii Ilyasa kwa maana ya
kwamba roho ya Nabii Ilyasa imemuingia yeye Hamza Issa na kwa hiyo yeye
wamekuwa Nabii Ilyasa” alisema Sheikh
Aliongeza
maelekezo na mafundisho ya uislamu yako wazi kuwa hakuna Mtume mwingine
katika Uislamu baada ya Mtume Muhammad (S.A.W) na kwamba upatikanaji wa
MTU ndani ya uislamu na kudai kuwa yeye ni Mtume ni kutaka kuamsha
hisia Kali za waislamu nchini.
“Baraza
la Ulamaa linapenda kuwafahamisha waislamu kwamba, yeyote atakayemfuata
mpotoshaji huyu atakuwa ametoka ndani ya uislamu” alisema Sheikh Mataka.
Pia
Baraza limetoa wito kwa Masheikh wa Mikoa, Wilaya na viongozi wa
taasisi mbali mbali za Kiislam kutotoa fursa ya aina yoyote kwa huyo
anayejiita Nabii ( Hamza Issa), ili kuzuia kuipotosha jamii.