PICHA KATIKA MATUKIO:VIJANA TARIME WAPAZA SAUTI KUTETEA MWANAMKE WAKIKURYA KUMILIKI MALI IKIWEMO ARDHI.

Vijana kutoka kata ya Turwa wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mdahalo juu ya masuala ya ukatili wa kijinsia kwa Mwanamke katika Wilaya ya Tarime wa pili kutoka kulia ni Afisa ulinzi  na usalama wa watoto CDF Sophia Temba mikono ni ishara ya nguvu ya pamoja katika kukomboa Mwanamke.

Maswali kwa ajili ya Mdahalo huo ulioandaliwa na CDF

Restuta Mpate Afisa Mradi Msaidizi  kutoka CDF akiendesha Mdahalo uliondaliwa na shirika la CDF Tarime.



Kundi la vijana Wilayani Tarime Mkoani Mara wamepaza sauti ya pamoja kwa lengo la kutetea Mwanamke pamoja na Mtoto wa kike kuwa nao wanahaki ya kumiliki Ardhi, Mali, kushiriki katika mikutano na  kufanya maamuzi na siyo kila kitu kinafanywa na Wanaume jambo  ambalo linazidi kupelekea Mfumo dume. 

Wakichangia mawazo  kupitia Mdahalo ambao umeandaliwa na shirika la Jukwaa la Utu wa Mtoto( CDF) chini ya Ufadhili wa Foundation for Civil Society mdahalo huo umefanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kata Turwa Mjini Tarime mkoani Mara kwa kushirikisha vijana 30 kutoka Mitaa yote ya kata ya Tuwa.

Sophia Temba ni Afisa ulinzi  na usalama wa watoto kutoka shirika la CDF amesema kuwa Shirika hilo lime lenga kuwafikia vijana 150 huku akieleza lengo la Mdahalo huo ni kusikiliza maoni ya wanaume kuhusu ushirikishwaji wa mwanamke katika jamii ya Kikurya ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo juu ya kupiga vita suala zima la ukeketaji.

Aidha Vijana hao wameweza kutoa Maoni ya nini kifanyike kwa lengo la kunusuru watoto wa kike ambao wanakumbana na suala zima la ukatili wa kijinsia ukiwemo ukeketaji na Ndoa za utotoni ambapo wamesisitiza suala zima la elimu kuendelea kutolewa katika jamii huska ili kutokomeza ukeketaji kwa mtoto wa kike.

Elimu itolewe katika shule za msingi na sekondari kupitia michezo, maigizo ili ujumbe ufike haraka wamesema vijana hao.









Nachingia kwanza sisi vijana tuwe mstari wa kwanza kutetea dada zetu ili wapate haki zao za msingi



Vijana  wakichangia mada mbalimbali katika mdahalo huo uliondaliwa na shirika la CDF nakufanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya kata Turwa mjini Tarime lengo ni kuzungumzia masuala mazima ya Ukatili wa kijinsia kwa Akina Mama, vijana hao wamepaza sauti ya pamoja kuwa Mwanamke nayeye anapaswa kumiliki Mali kama Mwanaume.


Afisa ulinzi na usalama wa watoto kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali Jukwaa la Utu wa Mtoto CDF Sopha Temba akiongea na CLEO24 NEWS Malengo ya Mdahalo huo.

Mdahalo unaendelea Restuta Mpate kutoka CDF anaongoza

Nachingia hoja




Afisa ulinzi na usalama wa watoto kutoka shirika lisilokuwa la kiserikali Jukwaa la Utu wa Mtoto CDF Sopha Temba akiongea na vijana kutoka kata ya Turwa ambao ni washiriki katika Mdahalo huo ulioandaliwa na shirika hilo.

Picha ya pammoja baada ya Mdahalo huo.

 PICHA ZOTE NA CLEO24 NEWS UKIWA NA HABARI NA MATUKIO PIGA SIMU NO 0766424928.

Powered by Blogger.