MASHABIKI, WANACHAMA YANGA WAANZA KUCHANGA, UONGOZI WAELEZA UTAKAVYOFANYA



Mashabiki wa Yanga wameanza kuonyesha mwamko kuichangia klabu yao baada ya ombi la uongozi kuwaomba wafanye hivyo.

Hata hivyo, uongozi huo umesema kila baada ya wiki utakuwa utakuwa ukitoa taarifa kuelezea kinachoendelea.

Ifuatayo ni taarifa iliyotolewa na uongozi wa Yanga, leo.

TAARIFA KWA UMMA:
Klabu ya soka ya Yanga SC kupitia Katibu Mkuu Charles Boniphace Mkwasa inashukuru sana kwani zoezi la uchangiaji toka kwa wanachama limekuwa zuri na likiendelea vyema.

Pia uongozi utakuwa ukitoa taarifa ya makusanyo kwa wanachama wake kila baada ya wiki moja ili waweze kufahamu mwenendo wa michango yao kwa klabu.

Klabu ina thamini mtu wa kipato chochote kuichangia klabu na kwa chochote unachotoa klabu inatanguliza shukrani za dhati na kutambua umuhimu wako katika mchakato huu.

Imetolewa na idara ya habari na mawasiliano; 
Young Africans SC


25/04/2017
Powered by Blogger.