WANANCHI WAKARIBISHWA KUTEMBELEA VITUO VYA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.



Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Edwin Ngonyani akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa maadhimisho ya siku ya hali ya hewa duniani mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi  akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa maadhimisho ya siku ya hali ya hewa duniani mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Edwin Ngonyani.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa maadhimisho ya siku ya hali ya hewa duniani mapema hii leo jijini Dar es Salaam.

Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dkt. Agnes Kijazi (hayupo pichani) habari wakati wa maadhimisho ya siku ya hali ya hewa duniani mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Picha zote na Eliphace Marwa


Na: Frank Shija
WATANZANIA wamepewa wito wa kutembelea Vituo vya hali ya hewa nchini ili kuona shughuli zitolewazo na Mamalaka ya Hali ya Hewa  ikiwa ni muendelezo wa kujifunza na kuongeza uelewa juu ya masuala ya hali ya hewa.
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhandisi Edwin Ngonyani wakati akitoa taarifa kuhusu maadhimisho ya siku ya Hali ya Hewa duniani ambayo inafikia kilele chake leo tarehe 23 Machi.
“Katika kuadhimisha siku hii ya hali ya hewa dunia ninatoa wito kwa wananchi kutembelea katika vituo vya hali ya hewa vilivyopo katika maeneo mengi ya nchi ili waweze kujifunza zaidi juu ya hali ya hewa na kuongeza uelewa hasa katika elimu juu ya mawingu,” alisema Mhandisi Ngonyani.
Aliongeza kuwa katika kuadhimisha siku hiyo mwaka huu  yamejikita katika kuongeza ulewa kwa wananchi kuhusu elimu juu ya Mawingu ambapo kauli mbiu yake ni, “Tuyaelewe Mawingu na Umuhimu Wake.”
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Hali ya Hewa(TMA), Dkt. Agness Kijazi amesema kuwa wananchi ni muhimu kujenga mazoea ya kufuatilia taarifa za hali ya hewa kwani ni muhimu katika shughuli za maendeleo.
Alisema maadhimisho ya mwaka huu yamepewa msukumo katika kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu sayansi ya Mawingu na mchango wake katika mzunguko wa maji kati ya nchi kavu, hali ya hewa ya muda mfupi na mrefu.
Maadhimisho hayo ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani uadhimishwa tarehe 23 machi kila mwaka yakiusisha nchi  191 ambazo ni wanachama wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani ikiwa ni moja kukumbuka kuanzishwa kwa Shirika hilo mnamo mwaka 1950.
Powered by Blogger.