Tumiieni mitandao ya kijamiii kuendeleza injili na maendeleo;


Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na IT Divisheni ya Africa Mashariki na Kati(ECD) Mch. Steven Bina akiwasilisha mada ya faida za matumizi ya mitandao ya kijamii katika semina ya Mawasiliano iliyoanza leo katika kanisa la SDA Tarime Central


Baadhi ya washiriki wa semina hiyo


Washiriki wa kanisa la Waadventista Wasabato(SDA)wametakiwa kutobaki nyuma katika kutumia  mitandao ya kijamii kuendeleza injili na masuala mengine muhimu kwa ajili ya maendeleo ya jamii .
Wito huo umetolewa leo na Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na IT Divisheni ya Africa Mashariki na Kati(ECD) Mchungaji Steven Bina wakati wa semina  ya mawasiliano  ambayo imeanza leo katika kanisa la SDA Tarime Central lililopo  Mjini  Mkoani Mara.
Mch. Bina amesema kuwa sio dhambi kutumia mitandao ya kijamii na kusisitza kuwa ina faida nyingi  ikitumiwa vizuri.
Semina hiyo ya siku tano imeandaliwa na Idara ya Mawasiliano Jimbo la  Mara( Mara Confrence))  ina lengo la kuhamasisha utumiaji wa mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kusambaza utume wa kanisa , kwa kujibu wa Mkurugenzi wa Idara hiyo Mchungaji Joseph Matongo.


Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa mara( mara regional press club) ambaye pia ni mwandishi wa gazeti la daily news mkoani mara mugini jacob akitoa mada kuhusu maandalizi ya habari bora katika semina ya mawasiliano liyoandaliwa na kanisa la sda jimbo la mara kupitia idara yake ya mawasiliano( global adventist internet network- gain). semina hiyo ya siku tano ina lengo la kuhamasisha utumiaji wa mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuendeleza injili na masuala mengine ya mandeleo

Wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na vyombo vya habari kanisa la SDA Jimbo la Mara Mchungaji Joseph Matongo

 

 


Powered by Blogger.