Makamu wa Rais Mh:Samia wanawake weka nguvu ya pamoja kupiga vita umaskini
Makamu wa rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo Jumanne Septemba 5,2017 amezindua tamasha la 14 la Jinsia mwaka 2017 lilirotaribiwa na TGNP Mtandao na Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia (GTI).
Tamasha hilo la siku nne linafanyika kuanzia Septemba 5 hadi 8,2017
katika Viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam huku mada
kuu ikiwa ni “ Mageuzi ya Mifumo Kandamizi Kwa Usawa wa Kijinsia na
Maendeleo Endelevu”.
Tamasha hilo la siku nne linafanyika kuanzia Septemba 5 hadi 8,2017
katika Viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam huku mada
kuu ikiwa ni “ Mageuzi ya Mifumo Kandamizi Kwa Usawa wa Kijinsia na
Maendeleo Endelevu”.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,Mheshimiwa Samia Suluhu alisema
serikali inatambua na kuthamini umuhimu wa uzingatiaji wa masuala ya
jinsia katika kuchangia kuharakisha maendeleo ya nchi.
“Serikali kwa kushirikiana na na wadau mbalimbali tumechukua hatua za
maksudi ili kuhakikisha tunajenga jamii yenye usawa wa kijinsia na
uwezeshaji wa wanawake kama ilivyoainishwa katika mikataba na maazimio
mbalimbali ya kimataifa”,alieleza Suluhu.
maksudi ili kuhakikisha tunajenga jamii yenye usawa wa kijinsia na
uwezeshaji wa wanawake kama ilivyoainishwa katika mikataba na maazimio
mbalimbali ya kimataifa”,alieleza Suluhu.
Alisema serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi,kusimamia
utekelezaji wa mipango na mikakati ya kuhakikisha wanawake na wanaume
wanashiriki kwa usawa katika kujiletea maendeleo pamoja na kunufaika na
maendeleo hayo.
utekelezaji wa mipango na mikakati ya kuhakikisha wanawake na wanaume
wanashiriki kwa usawa katika kujiletea maendeleo pamoja na kunufaika na
maendeleo hayo.
Mheshimiwa Suluhu alitumia fursa hiyo kuwaasa wanawake
kupendana,kunyanyuana,kufahamishana na kuelimishana na kupigania haki
zao kwa kuzingatia mila na desturi zao.
Aidha aliipongeza TGNP kwa harakati zake za kuiunga mkono na kuikosoa serikali pale wanapoona imekwenda tofauti.
Alisema kitendo cha kukemea na kutoa mapendekezo na suluhisho sehemu
ambayo wanaamini serikali haijafanya vizuri ni kitendo cha kiungwana na
kinachochea maendeleo ya taifa kwa ujumla.
ambayo wanaamini serikali haijafanya vizuri ni kitendo cha kiungwana na
kinachochea maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Aidha alizipongeza halmashauri za wilaya zinatoa asilimia 5 ya wanawake
huku akiwataka wazazi kutumia fursa ya elimu bure kupeleka watoto wao
shule ambapo takwimu zinaonesha kuwa kuna ongezeko kubwa la watoto wa
kike waliopelekwa shule mwaka huu.
huku akiwataka wazazi kutumia fursa ya elimu bure kupeleka watoto wao
shule ambapo takwimu zinaonesha kuwa kuna ongezeko kubwa la watoto wa
kike waliopelekwa shule mwaka huu.
Mbali na uzinduzi huo ameongoza zoezi la kutoa tuzo kwa baadhi ya
akinamama waliofanya vizuri na kutoa mchango katika maendeleo ya
wanawake.
akinamama waliofanya vizuri na kutoa mchango katika maendeleo ya
wanawake.
Awali akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi
alisema Tamasha la Jinsia ni Jukwaa la wazi la wanawake na wadau wa haki
za binadamu ambalo hufanyika kila baada ya mwaka mmoja likiratibiwa na
TGNP Mtandao lengo likiwa ni kushirikishana mafanikio,uzoefu,kuainisha
changamoto na kuweka mkakati wa kukabiliana na changamoto hizo.
alisema Tamasha la Jinsia ni Jukwaa la wazi la wanawake na wadau wa haki
za binadamu ambalo hufanyika kila baada ya mwaka mmoja likiratibiwa na
TGNP Mtandao lengo likiwa ni kushirikishana mafanikio,uzoefu,kuainisha
changamoto na kuweka mkakati wa kukabiliana na changamoto hizo.
Alisema Tamasha hilo linalofanyika kila mara baada ya miaka miwili
linaandaliwa na taasisi kadhaa zinazotetea haki na usawa wa jinsia
zikiongozwa na TGNP Mtandao na mwaka huu limeshirikisha wanawake zaidi
ya 1000 kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania.
linaandaliwa na taasisi kadhaa zinazotetea haki na usawa wa jinsia
zikiongozwa na TGNP Mtandao na mwaka huu limeshirikisha wanawake zaidi
ya 1000 kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania.
Aliongeza kuwa tamasha hilo linajikita katika kutambua mchango wa
wanawake ambao wamekuwa mfano katika kuchochea maendeleo katika ngazi ya
kitaifa na kimataifa lakini pia wanaume ambao wamekuwa mfano katika
kutetea ajenda ya haki za wanawake.
wanawake ambao wamekuwa mfano katika kuchochea maendeleo katika ngazi ya
kitaifa na kimataifa lakini pia wanaume ambao wamekuwa mfano katika
kutetea ajenda ya haki za wanawake.
“Malengo ya Tamasha hili ni kutafakari na kusherekea
mafanikio,kujadili changamoto na kuweka mikakati ya pamoja kutatua
changamoto hizo,kutathmini ushiriki wa wanawake katika michakato ya
kufanya maamuzi na katika ngazi ya uongozi",alifafanua.
mafanikio,kujadili changamoto na kuweka mikakati ya pamoja kutatua
changamoto hizo,kutathmini ushiriki wa wanawake katika michakato ya
kufanya maamuzi na katika ngazi ya uongozi",alifafanua.
"Malengo mengine ni kufuatilia,kuhifadhi, kutambua na kusherekea
viongozi wanawake wenye michango ya kuigwa juu ya usawa wa kijinsia na
uwezo wa wanawake hususani Mapambano dhidi ya mfumo dume na kuimarisha
harakati na nguvu za pamoja katika Ukombozi wa mwanamke”,aliongeza Liundi.
viongozi wanawake wenye michango ya kuigwa juu ya usawa wa kijinsia na
uwezo wa wanawake hususani Mapambano dhidi ya mfumo dume na kuimarisha
harakati na nguvu za pamoja katika Ukombozi wa mwanamke”,aliongeza Liundi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP, Vicensia Shule aliwataja na
kuwapongeza wanawake waliofanya vizuri maeneo mbalimbali ambapo Makamu
wa Rais alikabidhi tuzo kwa akina mama hao.
kuwapongeza wanawake waliofanya vizuri maeneo mbalimbali ambapo Makamu
wa Rais alikabidhi tuzo kwa akina mama hao.
Miongoni waliopokea tuzo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Tanzania, Bi.
Samia Suluhu, aliyekabidhiwa tuzo yake na Mwenyekiti wa bodi.
Samia Suluhu, aliyekabidhiwa tuzo yake na Mwenyekiti wa bodi.
Wengine ni pamoja na Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania, Anna Makinda,
Mbunge wa Bunda Mjini, Estar Bulaya, Mama Getrude Mongela, Dk. Ester
Mwaikambo, na Msanii Fatma Baraka (Bi. Kidude) kwa jitihada
walizozionesha katika uongozi na wote walipewa tuzo.
Mbunge wa Bunda Mjini, Estar Bulaya, Mama Getrude Mongela, Dk. Ester
Mwaikambo, na Msanii Fatma Baraka (Bi. Kidude) kwa jitihada
walizozionesha katika uongozi na wote walipewa tuzo.
Tamasha hilo limeandaliwa na mashirika mbalimbali ya wanawake na haki za
binadamu,watu binafsi na wadau wengine wakiwemo Wanaharakati Vijana
(YFF),Mtandao wa wanawake na Maji,Wanasemina za Jinsia na Maendeleo
(GDSS) na Vituo vya Taarifa na Maarifa.
binadamu,watu binafsi na wadau wengine wakiwemo Wanaharakati Vijana
(YFF),Mtandao wa wanawake na Maji,Wanasemina za Jinsia na Maendeleo
(GDSS) na Vituo vya Taarifa na Maarifa.
ANGALIA PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI HAPA CHINI
Makamu
wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (mwenye mtandio) akikata utepe
pamoja na wageni meza kuu kuashiria uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia
Tanzania la mwaka 2017
wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (mwenye mtandio) akikata utepe
pamoja na wageni meza kuu kuashiria uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia
Tanzania la mwaka 2017
Makamu
wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (mwenye mtandio) akikata utepe
pamoja na wageni meza kuu kuashiria uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia
Tanzania la mwaka 2017.
wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (mwenye mtandio) akikata utepe
pamoja na wageni meza kuu kuashiria uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia
Tanzania la mwaka 2017.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Bi. Lilian Liundi (kushoto) akimpongeza
Spika mstaafu mwanamke wa Bunge la Tanzania, Anna Makinda (kulia) mara
baada ya kupokea tuzo yake.

Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo Mama Getrude Mongela (kulia)
Spika mstaafu mwanamke wa Bunge la Tanzania, Anna Makinda (kulia) mara
baada ya kupokea tuzo yake.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo Mama Getrude Mongela (kulia)
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Bi. Lilian Liundi akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia Tanzania Mwaka 2017.
Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP, Vicensia Shule akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia Tanzania Mwaka 2017.
Washiriki mbalimbali katika tamasha hilo.
Wawakilishi wa nchi mbali mbali wakitoa salam zao katika tamasha hilo
Katibu
Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Bi.
Siaba Mkinga akizungumza katika uzinduzi wa Tamasha hilo.

Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Bi.
Siaba Mkinga akizungumza katika uzinduzi wa Tamasha hilo.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu akizungumza leo wakati
akizinduwa rasmi Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017. Uzinduzi huo
umefanyika katika viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam.

akizinduwa rasmi Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017. Uzinduzi huo
umefanyika katika viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu akizungumza leo wakati
akizindua rasmi Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017. Uzinduzi huo
umefanyika katika viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam. Kulia
kwake ni wageni waalikwa meza kuu.
akizindua rasmi Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017. Uzinduzi huo
umefanyika katika viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam. Kulia
kwake ni wageni waalikwa meza kuu.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo
mmoja wa wanachama waanzilishi wa TGNP, Bi. Marjorie Mbilinyi (kulia)
mmoja wa wanachama waanzilishi wa TGNP, Bi. Marjorie Mbilinyi (kulia)
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo kwa
Zipora Shekilango (kulia) kwenye uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia
Tanzania la mwaka 2017.
Zipora Shekilango (kulia) kwenye uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia
Tanzania la mwaka 2017.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo
mmoja wa wanachama waanzilishi wa TGNP, Bi. Marry Lusimbi (kulia) kwenye
uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017.

mmoja wa wanachama waanzilishi wa TGNP, Bi. Marry Lusimbi (kulia) kwenye
uzinduzi rasmi wa Tamasha la Jinsia Tanzania la mwaka 2017.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo
mwakilishi wa halmashauri ya Kishapu Stephen Magoiga kwa kufanikiwa
kutenga rasilimali fedha kwenye bajeti ya mwaka 2017/18 kuwezesha
wasichana upata taulo za kujihifadhi bure wanapokuwa kwenye hedhi wakiwa
shuleni.
mwakilishi wa halmashauri ya Kishapu Stephen Magoiga kwa kufanikiwa
kutenga rasilimali fedha kwenye bajeti ya mwaka 2017/18 kuwezesha
wasichana upata taulo za kujihifadhi bure wanapokuwa kwenye hedhi wakiwa
shuleni.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi tuzo mwakilishi wa halmashauri Kisarawe.
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu (kushoto) akikabidhi daktari wa kwanza mwanamke Tanzania, Dk. Ester Mwaikambo (kulia).
Makamu wa Rais Tanzania, Bi. Samia Suluhu akitembelea miradi mbalimbali
na shughuli za akinamama wanaharakati ngazi ya jamii za kujikwamua.
na shughuli za akinamama wanaharakati ngazi ya jamii za kujikwamua.
Washiriki wa Tamasha la 14 la TGNP Mtandao wakiwa katika tamasha hilo kwenye viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam
Wanawake washiriki wa Tamasha hilo wakicheza kwa furaha
Baadhi ya washiriki wa tamasha la 14 la mtandao wa kijinsia Tanzania (TGNP mtandao) wakiwa katika tamasha hilo
Wageni kutoka nchi mbali mbali
Wanahabari wakifuatilia tamasha hilo
Wanahabari kutoka mikoani walioshiriki tamasha hilo