Video: IGP SIRRO AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA,ASISITIZA VITENDO ZAIDI YA MANENO

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro kwa mara ya kwanza amefanya mazungumzo maalum na wanahabari jijini Dar es Salaam na kutangaza dau nono la Sh10 milioni kwa atakayetoa taarifa kuhusu mauaji ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga. 



“Niwaambie ukweli kuwa katika hili, maneno yatakuwa machache lakini vitendo vitakuwa vingi zaidi,” amesema katika mkutano huo.

Pia IGP Sirro amewatangazia kiama madereva wa bodaboda na kuwataka kuacha kuvunja sheria za barabarani kwa makusudi.

“Huu ni wakati wa kutii utawala wa sheria bila shuruti na nimeshaongea na makamanda wa polisi nchi nzima,” amesema 

Msikilize hapo chini akiongea
 
Powered by Blogger.