Rais Magufuli Aagiza TCU kutowachagulia Wanafunzi wa Elimu ya Juu Vyuo



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Hostel mpya 20 za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Hostel hizo leo Jijini Dar es Salaam. Hostel hizo zilizogharimu takribani sh. Bilioni 10 zilizotolewa kufuatia ahadi ya Rais Maguful,i ambapo ujenzi wake umefanya na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania ambapo linatarajiwa kutumiwa na wanachuo 3840.Kutoka Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa. Makame Mbarawa na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Rwekaza Mukandara (katikati).

Waziri wa Elimu, Sanyansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndarichako akizungumza  katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Hostel mpya 20 zilizojengwa kufuatia ahadi ya Rais Magufuli aliyoitoa mwezi Juni mwaka 2016. Ujenzi wake umetekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na kugharimu takribani shilingi bilioni 10, ambapo Hosteli hizo zinatarajiwa kutumiwa na wanachuo 3840. 

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa. Makame Mbarawa akiteta jambo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Rwekaza Mukandara wakati wa hafla ya uzinduzi wa Hostel hizo leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa. Makame Mbarawa akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda wakati wa hafla ya uzinduzi wa majengo mapya Hostel  za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo Jijini Dar es Salaam.

Kwa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikitumbuiza wakati wa hafla ya uzinduzi wa majengo mapya ya Hostel za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo Jijini Dar es Salaam.

Picha muonekano wa baadhi ya majengo mapya ya Hostel za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Hostel hizo zilizogharimu takribani sh. Bilioni 10 zilizotolewa kufuatia ahadi ya Rais Maguful,i ambapo ujenzi wake umefanya na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania ambapo linatarajiwa kutumiwa na wanachuo 3840.

Rais Magufuli akipewa maelezo kuhusu Majengo mapya ya Hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mara baada ya kuzindua rasmi hosteli hizo leo jijini Dar es Salaam.Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ,Msanifu Majengo Elius Mwakalinga.Kutoka kushoto ni Waziri wa Elimu, Sanyansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndarichako,Mke wa Rais, Mama Janeth Magufuli na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Rwekaza Mukandara.

Rais Magufuli akikata utepe wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa majengo mapya ya Hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo jijini Dar es Salaam. Hostel hizo zilizogharimu takribani sh. Bilioni 10 zilizotolewa kufuatia ahadi ya Rais Maguful,i ambapo ujenzi wake umefanya na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania ambapo linatarajiwa kutumiwa na wanachuo 3840.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba walipokutana katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Hostel mpya za Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) leo Jijini Dar es Salaam. Hostel hizo zilizogharimu takribani sh. Bilioni 10 zilizotolewa kufuatia ahadi ya Rais Maguful,i ambapo ujenzi wake umefanya na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania ambapo linatarajiwa kutumiwa na wanachuo 3840. Kulia ni Waziri wa Elimu, Sanyansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndarichako na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Rwekaza Mukandara (kulia).

Rais Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mara baada ya kuzindua rasmi majengo mapya ya Hosteli za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo jijini Dar es Salaam. Hostel hizo zilizogharimu takribani sh. Bilioni 10 zilizotolewa kufuatia ahadi ya Rais Maguful,i ambapo ujenzi wake umefanya na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) chini ya usimamizi wa Jeshi la Wananchi Tanzania ambapo linatarajiwa kutumiwa na wanachuo 3840.
Picha zote na: Frank Shija


Na: Lilian Lundo na Beatrice Lyimo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kutowachagulia vyuo wanafunzi wa elimu ya juu na kuwaacha wanafunzi hao kuchagua vyuo wanavyovitaka wenyewe.

Agizo hilo limetolewa leo, Jijini Dar es Salaam Rais Magufuli alipokuwa akizindua Mabweni mapya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa Chuoni hapo Juni, mwaka jana.

“Ninaamini kama wanafunzi wangepewa nafasi ya kuchagua vyuo wanavyovipenda wenyewe, vyuo vya Serikali kama vile Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Mzumbe vingekuwa na wanafunzi wengi sana,” alisema Dkt. Magufuli.

Aliendelea kwa kusema kuwa TCU imekuwa ikiwachagulia wanafunzi vyuo visivyo na sifa na makazi ya wanafunzi hivyo kusababisha wanafunzi hao kusoma katika mazingira magumu na wanapomaliza masomo yao hukosa ajira kutokana na vyuo hivyo kutokuwa na sifa.

Aidha, Rais Magufuli ameuagiza uongozi wa UDSM kutoza wanafunzi gharama ya shilingi mia tano(500) kama malipo ya makazi ya  mabweni hayo kwa siku badala ya shilingi mia nane(800) inayotozwa kwa mabweni mengine yaliyopo chuoni hapo.

Alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuwekeza katika elimu hivyo itahakikisha wanafunzi nchini wananufaika kwa kupata elimu bora kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu.
“watanzania walinichagua ili kutatua changamoto zinazowakabili na hivi ndivyo ninavyofanya kutatua changamoto hizo” alisema Rais Magufuli.

Naye, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amempongeza Rais Magufuli kwa kutoa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni hayo ambao kwa kiasi kikubwa yatatatua changamoto ya makazi iliyokuwa ikiwakabili wanafunzi wa chuo hicho.

Prof. Ndalichako amesema kuwa mabweni hayo yamejengwa kwa kipindi cha miezi 8 ambayo yatachukua wanafunzi 3840.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekaza Mukandala ametoa rai kwa wanafunzi wa chuo hicho kuhakikisha wanaimarisha usalama katika maeneo ya mabweni hayo na kulinda miundo mbinu yote iliyoweka.

“Ni lazima mzingatie matumizi sahihi ya kila kifaa kilichofungwa katika majengo haya, majengo haya ni mapya na yamejengwa kwa gharama kubwa kwa lengo la kutusaidia kuondokana na changamato iliyotukabili kwa muda mrefu,” alisema Prof. Mukangala.

Wakati huohuo Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi magomeni “QUARTERS”, mradi ambao kwa asilimia kubwa unawagusa watanzania wa hali ya chini.

Aidha Rais Magufuli ameendelea kusisitiza juu ya ahadi aliyoitoa kwa wakazi 644 waliokuwa wakiishi maeneo hayo kupewa nyumba ambapo wataishi bure kwa muda wa miaka mitano.

Pia, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) Msanifu Majengo Elvis Mwakalinga amesema ujenzi wa mradi huo umezingatia miundombinu yote iliyohitajika ambapo itakuwa na sehemu za makazi, biashara, maegesho ya magari na bustani ya kupumzikia.

Ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja ambapo ujenzi wake ulianza rasmi Octoba mwaka jana.
Powered by Blogger.