MASHABIKI SIMBA WALIOHARIBU UWANJA CCM KIRUMBA, HAWA HAPA
Baada ya Uongozi
wa Uwanja wa CCM Kirumba, kupitia Meneja wa Uwanja Steven Shija kutoa
taarifa ya mashabiki wa Simba kuharibu sehemu ya uwanja huo, baadhi ya
picha zimewanasa wakiwa katika uharibifu huo.
Mashabiki
wa Simba waliharibu uwanja huo kutokana na furaha waliyokuwa nayo baada
ya Simba kusawazisha mabao mawili na kufunga la ushindi ndani ya dakika
7 za mchezo.
Shija
alisema sherehe za mashabiki hao zilisababisha uharibifu mkubwa kwenye
maeneo ya kuingilia wachezaji, waamuzi na geti namba 4, eneo ambalo
walikuwa wamekaa mashabiki wa Simba.
Picha
zinaonyesha mashabiki hao wakirukaruka juu ya enero hilo la uwanja
wakati wakijua si eneo ambalo wanatakiwa kukaa watazamaji.
Mashabiki
wa Simba walionekana ni kama waliopagawa mara baada ya Simba kufunga
bao la tatu na la ushindi baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa
mabao 2-0.