Wadau wa Michezo Jitokezeni kudhamini michezo nchini – Nape



Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akiteta jambo na Mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu alipompokea na kumpongeza kwa kupeperusha vizuri bendera ya Tanzania katika mashindano hayo leo Jijini Dar es Salaam.

Katibu Mkuu kutoka Chama cha Riadha Tanzania Bw. Wilhelm Gidabuday akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumpokea na kumpongeza Mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu leo Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kumpokea na kumpongeza Mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu leo Jijini Dar es Salaam.

Mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kumpongeza leo jijini Dar es Salaam

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto)  akiangalia tuzo wakati akiipokea kutoka kwa mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu leo wakati wa hafla fupi ya kumpongeza jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati) akimpa mkono wa pongezi mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu baada ya pokea medali hiyo na kumvalisha leo wakati wa hafla fupi ya kumpongeza jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati) pamoja na mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu wakiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) tuzo aliyoipata Bw. Simbu katika mashindano ya Mumbai Marathon yaliyofanyika Januari 15 mwaka huu leo wakati wa hafla fupi ya kumpongeza jijini Dar es Salaam.
Picha/Habari na Genofeva Matemu
Wadau mbalimbali wa sekta ya michezo nchini wametakiwa kujitokeza kudhamini michezo nchini ili kuweza kurudisha utukufu wa mafanikio katika sekta ya michezo na nchi kwa ujumla.
Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye wakati wa hafla fupi ya kumpokea na kumpongeza mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za standard Chartered Mumbai Marathon 2017 leo Jijini Dar es Salaam.
“Wadau wa michezo jitokezeni tushirikiane kwa pamoja kuboresha michezo nchini na kurudisha utukufu wa mafanikio katika sekta za michezo na nyingine ninazozisimamia kwani ni sekta ambazo zina mvuto ndani ya jamii” amesema Mhe. Nnauye.
Aidha Mhe. Nnauye ameipogeza kampuni ya Multi Choice kwa kujitolea na kuwa wazalendo kuwekeza kwa mwanariadha Simbu ambaye amekua na mwanzo mzuri ambao utakua chachu kwa vijana wengi nchini kuthamini na kujituma katika mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za Standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Alphonce Felix Simbu amewataka wanariadha wenzake nchini kufanya juhudi katika mazoezi ili kufikia mashindano ya dunia ya riadha Tanzania itoe idadi kubwa ya washiriki katika mashindano hayo.
Naye Katibu Mkuu Chama cha Riadha Tanzania Bw. Wilhelm Gidabuday amempongeza mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za standard Chartered Mumbai Marathon 2017 Bw. Simbu na kumtaka kuendelea kuwa kioo kwa wanariadha wenzake nchini.
 
Powered by Blogger.