UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI NKOME VUTA NI KUVUTE



Wananchi wakiwa katika foreni ya uchaguzi kwenye Kata ya Nkome wilayani Geita ambapo kunafanyika uchaguzi mdogo wa diwani

Moja kati ya wananchi akimwelekeza mzee kuweka kura katika sanduku la kupigia Kura.
Msimamizi wa uchaguzi akimwekea harama ya kupiga kura kwenye kidole

Zoezi la uchaguzi likiendelea

Askari Polisi wakiimalisha ulinzi katika kituo cha kupigia kura.

Wananchi wakifatilia maelekezo kutoka kwa msimamizi wa kituo cha kupigia kura.

Moja kati ya wazee akiwa amepewa nafasi ya upendeleo ya kuchagua

Kijana akimsaidia mzee kupiga kura

Wasimamizi  wa uchaguzi wakiendelea na majukumu.


Jeshi la Polisi likizengea zengea mitaani katika kuakikisha swala la ulinzi na usalama linakuwepo katika mitaa hiyo.



Kata ya Nkome wilaya na Mkoa wa Geita,kumefanyika uchaguzi mdogo wa udiwani huku hali ya ulinzi na usalama ikitawala katika kipindi chote cha upigaji wa kura.
Madukaonline imezungumza na msimamizi mkuu wa uchaguzi ambaye ndie Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Geita,Ali Kidwaka ambapo ameelezea kuwa zoezi hilo limefanyika katika hali ya utulivu na kwamba jumla ya vituo therasini na nane (38)vimeusika kufanya uchaguzi.
“Zoezi la kupiga kura limeanza saa moja kamili ndio vituo vimefunguliwa na nimefanikiwa kuzungukia vituo vyote Therasini na nane  kwasababu uchaguzi unafanyika hapa Nkome katika vituo Therasini na nane na katika vituo nilivyozungukia hakukua na matatizo ya vivaa  na wananchi wameendelea kupiga kura kwa uhuru Kabisa”Alisema Kidwaka.
Kuhusu swala la ulinzi na usalama Kidwaka amesema kuwa hali ilikuwa tulivu hakuna fujo au usumbufu wowote ambao umeweza kujitokeza lakini nje ya vituo kuna maswala yalijitokeza ya uvunjifu wa amani na utulivu.
Madukaonline imezungumza na Baadhi ya wananchi wa kata hiyo,Hussein Omary ameeleza kuwa uchaguzi ambao umefanyika uko katika hali nzuri kwani hayupo ambaye ameshindwa kupiga kura vituo vyote vilikuwa wazi na kwamba kila mtu alikuwa ana uhuru wa kumchagua Yule ambaye anaona yupo sahihi kumwongoza.
Bi,Flora Mussa amesema kuwa wao kama wazee wanaishukuru serikali kwani hakuna buguza ambayo wamekutana nayo na kwamba wamekuwa wakipewa nafasi ya upendeleo na kuthaminiwa katika chumba cha uchaguzi.
Kwa mujibu wa msimamizi mkuu upigaji kura unatarajia kumalizika saa kumi kamili(10:00)na matokeo yatatangazwa Majira ya saa Moja kamili jioni(1:00)
IMEANDALIWA NA MADUKAONLINE
Powered by Blogger.