Simu ya mkononi nusura imtoe roho mke wa mtu Rorya






Mkazi wa Nyang’ombe kata ya Nyamagaro wilayani Rorya  mkoani Mara Joyce Akote (29) amenusurika kifo baada ya kunywa sumu kutokana na kukutwa na mume wake akiongea na simu ambayo mumewe aliitilia mashaka kuwa ya usaliti.

Akote alichukua maamuzi hayo magumu januari 21 baada ya mume wake kumtaka aeleze alikuwa akiongea na nani jambo ambalo alikataa kulitekeleza hivyo kuamua kutaka kujiondoa uhai.

  Ndevi Maziku ambaye ni mume wake alisema kuwa mke wake  aliamua kunywa sumu baada ya kuulizwa kuhusiana na simu ya mkononi,  na makosa aliyokuwa anayafanya wakati akipigiwa  alikuwa akitaka kuipokea alikimbia kujificha.

Maziku alisema kuwa hali hiyo ilikuwa inampa utata  na ndipo alipoanza kuhoji kulikoni lakini kikawa ni chanzo cha yeye kumtishia kuwa asimfuatilie .
“Ukiendelea kuniuliza uliza nitakuonyesha kitendo ambacho hutakisahau maishani mwako,  nikataka kujua kwa nini afanye vile lakini nikahisi kuwa alikuwa na mahusiano na mume mwingine nje,” alisema Maziku.

Hata hivyo baada ya kubainika kuwa amekunywa sumu alikimbizwa zahanati kunusuru maisha yake na kuokolewa  ndugu zake mwanamke walimfata ambapo mme wake hakutaka tena kurudiana na mke wake na hapa joto la asubuhi limezungumza na mwanaume huyo.

“Alisaga betrii akanywa, lakini namshukuru Mungu tulimkimbiza katka zahanati ya Nyamagaro tukaokoa maisha yake, na sasa amekimbia kwenda Kenya baada tu ya kupata fahamu,”alisema Maziku.

Hata hivyo Maziku alisema maisha yake na mke na wake tangu amuoe mwaka 2015 siyo mazuri kwani amekuwa hamsikilizi kama mume alikuwa akijiamulia nini afanye kwa wakati wake ambapo wakati mwingine alikuwa akiondoka bila hata kuaga.

Shuhuda  wa tukio hilo James Makanga alisema baada ya Akote kubainika kuwa amekunywa sumu alishiriki kumkimbiza zahanati ambapo alipata huduma ya kitabibu na kurejea katika hali yake ya uzima.

“Maziku ni jirani yangu, walikorofishana na mke wake ambaye alikunywa sumu tukamkimbiza zahanati ambapo alinyweshwa mziwa na kumwekea tripu ya maji, alipata fahamu akatoroka kurudi nyumbani na ndugu zake kutoka Kenya wakaja kumchukua,”alisema Makanga.

Mwenyekiti  wa kijji  cha Muharango  Jumanne Nyabori alisema kuwa alipopata taarifa ya tukio hilo alitoa maelekezo ya kwenda kituo cha polisi lakini hawakufanya hivyo.

“Matukio kama haya siyo mengi lakini wananchi wanapaswa kuwa makini na kuacha kuchukua maamuzi magumu kama haya ya kutaka kuondoa maisha yao, tunamsubiri arudi kutoka kwao ili sheria ifuate mkondo wake,” alisema Nyabori

 Wakati huo huku katika kijiji hicho aliyefaamika kwa jina la Pius Kuhuri mwenye umri wa miaka 17 mkazi wa kijiji cha Muhalango kata ya Nyamagalo Wilayani Rorya Mkoani Mara   amekutwa ameafrika dunia kwa kujinyonga na kamba ya katani ndani ya Nyumba

Chanzo cha tukio hilo hakijafaamika na tukio hilo ni la pili ndani ya Mwezi mmoja amesema diwani wa kata hiyo Ezra Masana.

Powered by Blogger.