Waziri
wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa
wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya kukagua chumba cha kuhifadhia abiria
kilichoteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo ,wa kwanza kulia ni Kaimu
Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi Bw. Gabriel Migire.(Picha na Benjamin Sawe)
Na: Benjamin Sawe
Serikali imeunda Tume ya uchunguzi ya watu 12 ili kuweza kuchunguza na kubaini
chanzo cha ajali ya moto iliyotokea jana saa Tano usiku katika chumba kidogo
cha kuhifadhia mizigo kilichopo kwenye jengo la Pili la abiria (Terminal II)
katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa Tume hiyo iliyoundwa inaongozwa na Joseph Nyahende ambae anatoka katika ofisi
za Makao Makuu ya Mamlaka ya Viwanja vya
Ndege nchini.
“Ninategemea
kupata ripoti ya kitaalamu kutoka kwa Tume hii, ili kutusaidia kubaini kiundani
juu ya chanzo haswa kilichopelekea moto huu”, amesema Waziri Mbarawa.
Aidha,
Waziri Mbarawa amefafanua kuwa huduma katika jengo hilo zinaendelea kama kawaida ambapo awali
zilisitishwa na kuhamishiwa katika Jengo la Kwanza la abiria (Terminal I).
“Mara
baada ya moto kutokea, kitu cha kwanza kilichofanyika ni kuudhibiti moto huu
ili usiweze kusambaa katika maeneo ambayo hayajaathirika, kisha tukatafuta njia
za kurudisha huduma kwa abairia”, amesisitiza Profesa Mbarawa.
|