Bao la kuongoza la polisi Mara
liliwekwa kimiani dakika ya 37 na Bauba Matagi na kuufanya timu hizo kuanza
kushambuliana kwa kasi hadi mapumziko polisi Mara ilikuwa ikiongoza kwa bao
1-0.
Katika kipindi cha pili timu zote
zilianza mashambulizi ya hapa na pale kwa zamu na hadi dakika ya 78 Polisi Mara
iliongeza bao la pili kupitia kwa Moses Said aliyekuwa ameingia dakika mbili
zilizokuwa zimepita.
Bao la pili la Polisi Mara
liliwafanya mashabiki na viongozi wa timu hiyo kunyanyuka kwenye viti vyao
kuonyesha furaha ya kupata ushindi huo.
Kocha mkuu wa Polisi Mara, Henry
Mkanwa alisema kikosi chake kinaendelea kuimarika siku hadi siku kutokana na
kazi kubwa anayoifanya ya kukinoa.
Alisema wadau wa soka mkoani mara
wategemee kuona timu hiyo ikiimarika zaidi katika michuano ya ligi daraja la
kwanza hasa ikifanya vizuri zaidi musimu ujao.
“Hatutashuka daraja kama ilivyokuwa
inasemwa na wadau na mashabiki wetu baada ya kufanya vibaya katika mzunguko wa
kwanza na mwanzo wa huu wa pili,”alisema Mkanwa.
Kocha wa viungo wa Rhino Rangers,
Dan Murumbe alikubaliana na ushindi wa Polisi Mara huku akisema makosa
yaliyofanywa na mabeki wa timu yake ndiyo yaliyoigharimu.
“Ushindi ulikuwa wa halali,
tumetolewa F.A kutokana na mfumo uliopo wa ukipigwa unatoka, nasi tumetoka
tunaenda kujiandaa na ligi daraja la kwanza,”alisema Murumbe.
Akizungumza kwa niaba ya mashabiki
wa Polisi Mara, Khalid Opec alisema timu hiyo imeanza kurudisha mashabiki wake
na itafikia malengo ya mkoa kuwa timu bora.
“Kwa sasa tunaona Polisi Mara
inaanza kutuonyesha kuwa makocha wanafanya kazi, chama cha soka na ofisi ya
mkoa maleno yao yaweza kutimia kuiinua timu hii,”alisema Opec.
Mwisho.