JESHI LA POLISI LINAWASHIKILIA WATU KUMI KUHUSU TUKIO LA VIDEO ILIYOSAMBAA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII IKIONESHA MAMA AKIPIGWA VIBOKO.


Baada ya kusamba video katika mitandao ya kijamii ikionyesha akipigwa viboko na wanaukoo  Mama mmoja  Mwenye umri wa miaka 38 Msimbiti na Mkulima  mkazi kitongoji cha Migutu, kijijicha Kinesi Kata ya Nyamunga Wilayani Rorya Mkoani Mara jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Tarime Rorya Tayari linashikilia watuhumiwa kumi kuhusiana na tukio hilo na kati ya hao watuhumiwa watano ni viongozi wa balaza la Mila akiwemo Mwenyekiti  na wajumbe wake Wanne n watuhumiwa wengine ni wale walioshiriki kumshika na kumlaza  mhanga wa tukio hilo ili aweze kuadhibiwa.



Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Tarime Rorya Andrew Satta amesema kuwa tukio hilo lilitokea Januari 23 Mwaka jana  Majira ya saa kumi na Moja jioni  katika Eneo la Mastooni lililopo kitongoji cha Migutu, kijiji cha Kinesi Kata ya Nyamunga Wilayani Rorya Mkoani Mara,


Aidha Kamanda alisema kuwa Mtu Mmoja mwenye Umri wa miaka 38 Msimbiti Mkulima na mkazi wa kijiji cha Kinesi ambaye ni Mhanga wa tukio hilo liliosambaa katika mitandao ya kijamii akipigwa viboko na watu sita  ambapo watu hao waliamulishwa kumuchapa viboko na wajumbe wa kumi wa baraza la mila la kabila la wasimbiti liitwalo Irienyi ndodo baada ya  kulalamikiwa na kupelekwa katika balaza hilo baada ya kumkana mama yake mazazi   mwenye umri wa 55 huku akimtuhumu kwa uchawi.


Kutokana na mama kuripoti kwa wajumbe wa balaza ndipo waliamulu mama huyo kupigwa viboko  makalioni  hivyo mpaka saas wathumiwa kumi wanashikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na tkio hilo huku wengine wakiendelea kusakwa kwa lengo la kuwafikisha mahakamani ili kujibu suala hilo.


Watuhumiwa wote wanaendelea kuhojiwa na watafikishwa mahakamani mara moja kijibu shitaka linalowakabili huku jamii ikilaani vikali unyama huo ulifanyika

Powered by Blogger.