AUA KAKA YAKE KWA KUCHELEWA KUPIKA


Mkazi wa  kitongoji cha Bondeni, kijiji cha Mpakani katika mji mdogo wa Sirari Nandi Lula (19) anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumchoma kisu kaka yake, Masuke Lula (25) na kumsababishia kifo kutokana na kuvuja damu nyingi.

Kamanda wa mkoa wa Polisi,Tarime/Rorya Andrew Satta amedhibitisha kutokea kwa tukio hila na kusema kuwa amesema tukio hilo lilitokea usiku wa Januari 30 kwa marehemu aliemtaja kuwa ni Masuke Lula (25) aliyeanzisha ugomvi kwa mgodo wake Nandi Lula (19) kwa kuchelewa kuandaa chakula na kuanza kumgombeza.

Satta ameongeza kuwa jamii inapaswa kuwa makini na kutumia busara ili kuepusha madhara na vifo vizivyo tarajiwa kama hiki ambacho kilitokana na kumgombeza mdogo wake hivyo kumsabaishia apandwe hasira na kumuua kaka yake.

Shuhuda wa tukio hilo,Willison Patrick alisema  baada ya marehemu kufika nyumbani huku amelewa alimkuta mdogo wake akikatakata nyanya kwa ajili ya kupika mboga na kuanza kumgombeza ambo ambalo lilichochea hasira kwa mdogo wake.

Mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Mji wa Tarime, Samwel Malindi    amekiri kuupokea mwili wa marehemu na kuwa umehifadhiwa kwa ajili ya kusubiri taratibu za maziko zifanywe na ndugu wa marehemu.






Powered by Blogger.