MKUU WA MKOA MARA AMASISHENI WANANCHI KUJIUNGA NA MIFUKO YA BIMA YA AFYA

MKUU WA MKOA WA MARA CHARLES MLINGWA AKIONGEA NA WATUMISHI WA HUDUMA YA AFYA JANA KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA TARIME KULIA KWAKE NI MKUU WA WILAYA YA TARIME GLORIOUS LUOGA KUSHOTO KWAKE NI MKURUGENZI WA ALMASHAURI YA MJI WA TARIME ELIAS NTIRUHUNGWA.

WAHUDUMU WA AFYA WAKISIKILIZA MKUU WA MKOA WA MARA



Mkuu wa mkoa wa Mara Charles Mlingwa amewataka Viongozi wa serikali na  na watendaji wa Vijiji na Kata  kuendelea kuamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kuweza kupata matibabu huku wakiunganisha familia zao kwa lengo la kuwapunguzia mlolongo wa kulipa fedha nyingi pale wanapohitaji huduma ya Afya katika Hospitali.

Hayo yamebainishwa kipindi mkuu wa mkoa huyo akiongia na Wahudumu wa Afya Hospitali ya Halmashuri ya mji wa Tarime Mkoani Mara huku akiwataka watumishi hao kuendelea kuwa na maadili ya kazi na kuboresha utendaji kazi kwa lengo la kuletea wananchi maendeleo.

Mlingwa alisema kuwa endapo wananchi wataweza kjiunga katika mifuko ya bima ya Afya itawasaidia kuhakikishia wanapata Huduma ya Afya mahali popotea bila ya usumbufu.

Aidha mkuu wa mkoa alisema kuwa serikali tayari imejipanga kwa lengo la kuendelea kutatua changamoto zinazokabilia idara ya Afya zikiwemo sare pamoja na upungufu wa madawa katika Hospitali za serikali.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa amezidi kuwataka wahudumu wa Afya kuendelea kuwa wazalendo  kwa kuwahudumia wananchi vizuri huku wakiondokana na visingizio  huku wakitumia kauli ya Hapa kazi tu kwa vitendo na kuchukua hatua kwa spidi huku wakitumia utalaamu wao kwani mgonjwa anahitaji huruma kwani serikali inatambua uwepo wao.

Aidha Mkuu wa Mkoa huyo ameweza kuzungumzia mikakati aliyonayo kuhakikisha anatatua changamoto ya Maji safi na salama mbali na kuwa karibu na Ziwa Victoria  ambapo alisema kuwa hivi karibuni anatarajia kuwa na kikao cha wadau ili kuzungumzia suala zima la maji.

Hata hivyo Mlingwa amezidi kumpongeza mkuu wa wilaya ya Tarime Glorious Luoga kuendelea kusimamia suala zima la Amani ikiwemo uboreshaji sekta ya Afya pamoja na usimamizi wa kutekekteza  madawa ya kulevya Bangi ambazo zinalimwa na wananchi ikiwa ni pamoja na kuendelea kusimamia vyema suala zima la Amani.
WAKITEMBELEA MAZINGIRA YA HOSPITALI HALMSHAURI YA MJI WA TARIME
 

Powered by Blogger.