HALMASHAURI YATOA MILLIONI MOJA LAKI NNE KWA WAHANGA WA MOTO

WATATU NI MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME MOSES MISIWA YOMAMI AKIKABIDHI FEDHA KWA MMOJA WA WAHANGA WA NYUMBA ZILIZOUNGUA NYAMONGO JANA WA KWANZA KUSHOTO NI KAIMU MKURUGENZI HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME PETER NYANJA AKIFUATIA KATIBU WA MBUNGE MRIMI ZABRON JIMBO LA TARIME VIJIJINI
WAHANGA WAKISILILIZA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME YOMAM
Halmashauri ya wilaya ya Tarime mkoani Mara imetoa shilingi millioni moja na laki Nne kwa kaya 11 zilizoathilika na suala la kuungua Nyumba 15 katika kitongoji cha Nyabikondo kijiji cha Kewanja kata ya Kembambo Nyamongo Wilayani Tarime mkoani Mara ili wanachi waweze kumalizia ujenzi  wa Nyumba hizo ili kuondokana na hadha ya Mvua ambazo zimeanza kunyesha

Wakipokea fedha hizo kutoka kwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Moses Misiwa Yomani wananchi hao wamezidi kutoa shukrani kwa serikali kwa kuona umhimu wa kutoa fedha hizo ili ziweze kuwasaidia

“Kuna baadhi ya kaya zetu ziliweza kuungaua na kila kitu kuungua ndani zikiwemo Sare za shule za wanafunzi sasa hii fedha itasaidia ka kiasi kikubwa kuweza kununua mahitaji muhimu baadhi yetu tutamalizia ujenzi ili kuepukana na Mvua ambazo zimeanza kunyesha” walisema Wananchi.

Akikabidhi Fedha hizo kwa wahanga wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Moses Misiwa alisema  kuwa suala hilo limepatiwa ufumbuzi baada ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pamoja na mkurugennzi kutembelea maeneo hayo na kutoa fedha hizo ili kuwasaidia kumalizia ujenzi.

Misiwa  alisema kuwa Halmashauri imekaa na kuona kutumia vyanzo vya mapato ya Ndani ili kuweza kutoa kiasi hichi cha fedha kwa lengo la kuwasaidia wanachi ambao waliweza kuathilika na moto ambao ulikuwa ukichoma Nyumba hivyo bila kujua chanzo chake katika kitongoji cha Nyabikondo na Kemambo Nyamongo.

Kwa upande wake Mtendaji wa kijiji cha  Kewanja Sumun Samson  amesema kuwa suala hilo la nyumba kuungua zenyewe lilichukua takribani  Tangu septemba Tano mpaka kumi na tatu siku sita  bila kupatiwa ufumbuzi huku zikungua jumla ya Nyumba 15 katika kaya 11 hadi sasa suala hilo limeisha huku akizidi kuwaomba wanachi kuendelez ushirikiano ili kudumisga suala la amani

Naye Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya wilaya ya Tarime Peter Nyanja alisema  kuwa fedha hizo zimetolewa kwa ajili ya kutimiza ahadi iliyohaidiwa na Mkurugenzi pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga baada ya kuwatemmbelea wahanga hao.

Zabron mrimi ni katibu wa Mbunge jimbo la Tarime vijiji alisema kuwa suala la kuungua kwa nyumba hizo watoto wawili  wa Familia moja waliweza walipata majeraha ya moto na mpaka sasa hali zao ni Nzuri ambapo ofisi ya mbunge iliweza kutoa msaada wa godoro tano pamoja na Mchele kwani baadhi yao vyakula viliweza kuungua ndani


MTENDAJI WA KJIJI CHA KEWANJA SUMUN SAMSON AKIONGEA NA WAHANGA WA MATUKIO NYAMONGO

 
MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME YOMAM AKITETA JAMBO NA MTENDAJI WA KIJIJI CHA KEWANJA SUMUN SAMSON KULIA.
Powered by Blogger.