WANANCHI WA KIJIJI CHA KEWANJA WALILIA VONGOZI WA DINI NA SERIKALI.

WANANCHI WAKICHANGIA HOJA KATIKA MKUTANO HUO

WANANCHI WAKICHANGIA WAHANGA WA MOTO KATIKA KIJIJI CHA KEWANJA NYAMONGO
WANANCHI WAAKICHANGIA HOJA KUHUSU SUALA ZIMA LA MOTO NA NINI KIFANYIKE.
OCD NYAMWAGA MORRIS OKINDA AKIONGEA NA WANACI WA KIJIJI CHA KEWANJA KATIKA MKUTANO WA HADHARA.
MWENYEKITI WA KIJIJI CHA KEWANJA TANZANIA OMUTIMA AKIONGEA NA WANANCHI WAKE KATIKA MKUTANO WA HADHARA

KIJANA MMOJA ALIYEJULIKANA KWA JINA LA GASPAL AKISHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUJIUSISHA NA SUALA LA UGANGA KATIKA KIJIJI AMBACHO KIMEKUMBWA NA JANGA LA MOTO.


Baada ya kuendelea kutokea kwa matukio ya kulipuka kwa moto na kuunguza nyumba za wananchi katika kitongoji cha Nyabikondo kijiji cha kewanja kata ya Kemambo Nyamongo Wilayani Tarime Mkoani Mara wananchi wameimba serikali kutoa msaada wa haraka ili kunusuru wahanga hao huku viongozi wa dini kupitia madhehebu yote kuingilia kati ili kutoa msaada wa kiroho ili suala hilo la kuungua kwa moto kijijini hapo liweze kuisha mara moja.

Hayo yamebainishwa na wanachi katika mkutano wa kijiji uliofanyika kijiji cha Kewanja Nyamongo juu ya kujadili suala zima la kuungua kwa Nyumba ambapo sasa zimeisha ungua Nyumba 14 zikiwemo za nyasi 11 na za bati 4 huku watoto Wanne wakijeruhiwa kwa moto jambo ambalo limewanyima amani wanachi hao na kupelekea kulala nje kwa kuhofia moto huo.

Nicodemus Keraryo ni mmoja wa wanachi akitoa maoni katika mkutano huo kuhusu suala zima la kulipuka kwa moto alisema kuwa viongozi wa dini kupitia madhehebu yote hawana budi kuingilia kati kwa ajili ya kutoa maombi ili suala hilo kumalizika.

“Watu tunapaswa kufunga toba na kushirikiana na viongozi wa dini kijijini hapa na kuweka kambi katika kitongoji ambacho kimeathilika sana ili kuombea wahanga wa matukio na mwenyezi mungu atasikiliza kilio chetu" Alisema Keraryo.

Tanzania Omutima ni Mwenyekiti wa kijiji cha Kewanja  amezidi kuwasihi wanachi kuendelea kutoa taarifa ili kuweza kubaini chanzo cha Moto huo huku akiwakikishia suala zima la ulinzi na usalama na kuaidi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi katika kukomesha suala hilo.
“Wananchi endeleeni kuchukua taadhali kubwa sana juu ya matukio haya ambayo yanazidi kutushangaza wakazi wote wa Kewanja” alisema Omutima.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kitongoji cha Nyabikondo  Nelson Nyangi amesema kuwa mpaka sasa tayari zimeungua Nyumba 14 hivyo ameiomba serikali kutoa msaada wa haraka ili kuokoa watoto wadogo wanaolazwa nje,

Morris Okinda ni Ocd Kituo cha Polisi  Nyamwaga amlisema kuwa suala la kuchoma Nyumba mchana ni kosa kubwa sawa na mauaji  na jeshi la polisi halitafumbia macho  jambo hilo huku akilaani vikali wanganga wa kinyeji ambapo kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Gaspa anashikilwa na jeshi la polisi kwa kujiusisha na suala la uganga.
“Sasa nitazunguka nyumba kwa nyumba kwa ajili ya kusaka waganga wa kinyeji ambao ni wacoichezi wenda nyie ndiyo munachoma kwa ajili ya kupata wateja na wewe kijana lazima baada ya mkutano huu niende na wewe kwa ajili ya kuwataja wenzako” alisema Okinda.

Hata hivyo katika mkuatano huo imeweza kuendeshwa changizo kwa ajili ya wahanga wa matukio hayo ambapo zimepatikana zaidi ya shilingi laki mbili.

……Mwisho…











Powered by Blogger.