WANAWAKE RORYA TUTAENDELEA KUZAA HUDUMA YA MAJI TUMEPATA.

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA GEORGE JACKSON AKIMUTWISHA NDOO YA MAJI MMOJA WA WANANCHI BAADA YA KUZINDUA RASMI MRADI WA KISIMA CHA MAJI KIJIJI CHA KISUMWA WILAYANI RORYA MKOANI MARA.



KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AKINYANYUA NDOO YA MAJI BAADA YA KUZINDUA RASMI MRADI HUO WA MAJI KIJIJI CHA KISUMWA WILAYANI RORYA MKOANI MARA


Wanawake wilayani Rorya mkoani Mara wamesema kuwa wataendelea kuzaa vyema baada ya kuondokana na hadha ya huduma ya maji suala ambalo lilikuwa ninawalazimu kuamuka majira ya ya usiku na kuwaacha waume zao wakiwa wamelala huku wakitembea umbali mrefu kwa ajili ya kupata maji
Hayo yamebainishwa hivi karibuni kipindi Mwenge wa uhuru ulipokuwa ukizindua mradi wa maji  katika kijiji cha kisumwa wilayani Rorya mkoani Mara ambapo mradi huo wa maji umegalimu shilingi millioni 633 huku ukitarajia kuhudumia idadi ya watu 2618 sawa na kaya 524

Wakina mama ao walidai kuwa kitendo cha hadha ya maji katika kijiji cha Kisumwa kimewakumba kwa muda mrefu suala ambalo lilikuwa linapelekea wanawake kuamka usiku  na kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kutafuta huduma ya maji na kushindwa kulala na aume zao mpka asbuhi.

“Maji hapa yalikuwa ni kero kubwa hatulali na wanaume zetu tunatembea umbali mrefu wakati mwingine wengine wanatishiwa kubakwa kwani ni usiku wa manane hautfurahia ndoa zet sasa tutazaa kwa wingi kwa sababu maji yametufikia karibu” walisema kina mama hao.

Emmanuel Masanja ni Mwandisi wa maji Wilayani Rorya Mkoani mara alisema kuwa mradi huo ni Miongoni mwa miradi mikubwa inayotelezwa chini ya mfumo wa Tekeleza sasa kwa matokeo makubwa ambapo alisem akuwa unatariajia kuhudumia watu2618 sawa na kaya 524.

Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za mwenge kitaifa George Jackson amewataka wanachi wilayani rorya mkoani mara kuendelea kulinda  miundombinu pamoja na vyanzo vya maji nakuondokana na suala la kuharibu miundombinu kwa ni suala hilolinachangia kurudisha naendeleo nyuma.
Pia amewataka wakulima wa kilimo cha umwagiliaji Chereche kuendelea kulinda vyanzo vya maji na kuendelea na umoja wao katika kudumisha kilimo hicho.

Hata hivyo kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa amewataka vijana kuondokana na suala la kuchagua kazi huku wakibagua kilimo bali wajikite katika suala zima la kilimo huku wazazi na walezi Mkoani Mara wakitoa ushirikiano mkubwa kwa walimu wa shule za msingi na sekondari ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi hao.
Mwaka huu kauli mbiu ya mwenge wa uhuru Vijana ni Nguvu kazi ya Taifa washirikishwe na kuwezeshwa



Powered by Blogger.