MADIWANI HALMASHAURI YA TARIME WAJITOKEZA KUPIMA VIRUSI VYA UKIMWI.

DIWANI WA KATA YA BINAGI AKIPIMA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI HII LEO
DIWANI WA KATA YA NYARERO MHABASI AKIPEWA KARATASI YENYE NAMBA KWA AJILI YA KUPIMA
MMOJA WA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME AKIPIMA HII LEO
DIWANI WA KATA YA KEMAMBO AMBAYE PIA NI MWENYEKITI WA CCM WILAYA YA TARIME RASHID BUGOMBA AKIPIMA




Ili kuweza kuhamasisha wananchi Wilayani Tarime mkoani Mara waweze kujitokeza kwa lengo la kupima maabukizi ya Virusi vya Ukimwi ili kujua Afya zao na kuanza kutumia dawa za ARV, Madiwani katika Halmashari ya Wilaya ya Tarime mkoani Mara wamejikeza kupima maambukizi ya virusi vya ukimwi kabla ya kuanza baraza la madiwani la kawaida kwa lengo la kujua Afya zao ili kuwa mabalozi wazuri katika vijiji na kata kwa lengo la uahamasisha wananchi kujitokeza kupima.

Zoezi hilo limeendelea hii leo kabla ya kuanza kikao cha baraza la madiwani ambapo madiwani hao wamejikokeza kwa wingi kwa lengo la kupima ili kujua afya zao ambapo katika kikao kilichoisha madiwani hao waliweza kuazimia kupima wote wakiwemo watumishi wa Halmashauri ili kuweza kujua Afya zao.

John Mhabas ni diwani kata ya Nyarero ambaye pia alileta hoja hiyo ya madiwani kujua Afya zao katika balaza la madiwani lililopita alisema kuwa suala zima la kupima ni jukumu lao kama viongozi wa wananchi ili kuweza ili kuweza kuwa mabalaozi wazuri katika sula zima la kuhamaisha upimaji wa maambukizi ya virusi vya ukimwi.

Aidha Mhabas aliongeza kuwa endapo diwani yeyote atakutwa ameambukizwa Virusi vya ukimwi ataweza kuunda kikundi na kuweza kuhamasisa wagonjwa wengine ili kuendelea kutumia dawa za kulefusha maisha ili kuendelea kuishi.

 Moses Yomamami nimwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime amesema kuwa maendeleo yeyote yanayofanywa na kiongozi lazima aweze kuwa na afya iliyonjema hivyo suala la afya limewalazima kupima ili kuweza kujua afya baada ya kuazimia japokuwa sheria ya kupima virusi vya ukimw ni kupima ni hiari ya mtu na siyo kulazimishwa japokuwa wao kama madiwani waleweza kuazimia na kuweza kutimizza zoezi zima.

Naye Veronica Sando diwani wa viti maalumu CHADEMA aliongeza kuwa suala zim ala kupima limemufuraisha kwa madiwani wenzake kujitokeza kupima huku akisema ugonjwa Ukimwi ni kama ugonjwa Mwingine hivyo suala zima la kupima kwa madiwani hilo ni chachu kubwa kwani madiwani wakianza kuhamasisha wananchi bila kupima zoezi litakuwa gumu.
DIWANI WA VITI MAALUMU CHADEMA AKIPEWA MAELEKEZO NA KATIBU WA AFYA WILAYA YA TARIME NEEMA ALPHONCE
 

Powered by Blogger.