ACACIA WAKABIDHI BILLIONI 1.3 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME USHURU WA HUDUMA.

MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME MOSES MISIWA YOMAMI AKIWA NA MFANO WA HUNDI YA SHILINGI BILLIONI 1.3 ZILIZOTOLEWA NA MGODI WA UCHIMBAJI WA DHAHABU NYAMONGO ACACIA KULIA WA KWANZA NI MENEJA MSADIZI WA ACACIA JOHN CONNELL ANAYEFUATIA NI MKUU WA WILAYA YA TARIME GLORIOUS LUOGA WA KWAZNZA KULIA NI MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME APOO CASTRO TINDWA.
MENEJA MSADIZI ACACIA JOHN CONNELL AKIKABIDHI MFANO WA HUNDI YA BILLIONI 1.3 KWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME MOSE YOMAMI WA KWANZA KULIA NI AFISA MAHUSIANO ZAKAYO KAREBO




Mgodi wa dhahabu wa Acacia uliopo nyamongo wilayani Tarime mkoani mara umekabidhi hundi yenye thamani ya shilingi bilioni 1.3 Fedha za mrahaba kama ushuru wa huduma (service Levy) kwa serikali katika halmashauri hiyo kwa ajili ya fedha hizo kwenda kufanya maendeleo ya wananchi  ikiwemo huduma ya Afya Elimu Maji na barabara.

Akipokea hundi hiyo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Tarime mkoani mara  Moses Yomami amebainisha kuwa fedha hizo zitaelekezwa mojakwa moja katika shughuli za wananchi ikiwemo kufanya maendeleo ikiwa ni pamoja na mgodi huo kuongeza fedha za mrahaba huo baada ya halmashauri kuhoji jumla ya fedha zinazozalishwa na mgodi huo kwa muda wanotoa fedha hizo .

Glorious Luoga ni mkuu wa wilaya ya Tarime ameihakikishia halmashauri hiyo kusimamia na kuhakikisha fedha hizo zinafanya kazi kwa uhakikia huku akitoa kalipio kali kwa wataaakao hujumu fedha hizo na kusema kuwa wataweza kufikishwa mahakamani pale watakapobainika ili kurudisha fedha za serikali.

Kwa upande wake kaimu meneja wa mgodi wa Acacia uliopo nyamongoWilayani Tarime Mkoani mara John Connell amesema kuwa fedha hizo za mrahaba hazina budi kulekezwa kwa wananchi ili waweze kujua mgodi huo unatoa fedha hizo ikiwa ni pamoja na kutekeza miradi ya wanachi ili kujivunia uwepo wa mgodi huo.

 
MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME APOO TINDWA AKITOA SHUKRANI ZAKE KWA MENEJA MSAIDIZI ACACIA. 
Powered by Blogger.